Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 61 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 512 2021-06-29

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa kipande cha barabara ya lami kilichoanzia Sanya Juu kuelekea Kamwanga ambayo kwa sasa imeishia Kijiji cha Elerai wakati zimebaki takribani kilometa 44 kuunganisha na kipande kingine cha lami kilichotoka Tarakea na kuishia Kijiji cha Kamwanga?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushkuru, kwa niaba ya Waziri Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Steven Lemomo Kiruswa, Mbunge wa Longido, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Bomang’ombe – Sanya Juu – Kamwanga yenye urefu wa kilometa 97.2 kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami imekamilika. Ujenzi umepangwa kutekelezwa katika awamu tatu. Ujenzi katika awamu ya kwanza (Lot 1) wa sehemu ya Sanya Juu - Elerai kilometa 30.2 umekamilika. Serikali inatafuta fedha za kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa awamu ya pili (Lot 2) wa sehemu ya Elerai - Kamwanga kilometa 42 na awamu ya tatu (Lot 3) ya Bomang’ombe – Sanya Juu ambayo ni upanuzi wa barabara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati Serikali ikiendelea na juhudi za kutafuta fedha za ujenzi wa barabara tajwa, barabara hii itaendelea kufanyiwa matengenezo mbalimbali ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya shilingi milioni 728.878 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali.