Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Iringa Mjini hadi Kilolo ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika ahsante sana, kwanza nishukuru sana kwamba wakati wa kuchangia Mpango nilielezea kutokurudhishwa kuhusu mkandarasi aliyekuwa anaweka ile lami ya kilometa 10 na amebadiliswa na speed yake sasa yule anaeendelea kwa kweli ni nzuri na inaridhisha.

Sasa maswali yangu, kwa sababu ukiangalia kuna Project ya World Bank ambayo barabara hii kilometa zote 33.6 zilikuwemo na ninafahamu kwamba Waziri wa Fedha alisaini mkataba na hawa watu wa World Bank kwa ajili ya hiyo project. Je, upatikanaji wa fedha hizo utaondoa huo ujenzi wa awamu na kufanya barabara hii iweze kujengwa yote na kukamilika?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, Waziri atakuwa tayari kuambatana pamoja na mimi kwenda kuangalia hasa maeneo ya milimani kwa barabara hii ambayo hayapitiki ili tuweze kupata ufumbuzi na wananchi waweze kupita vizuri?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Justin Lazaro Nyamoga, Mbunge wa Kilolo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru kwa kutambua jitihada za Serikali na kwamba ni sikivu, alichokiomba tumeshakitekeleza kama Wizara. Pia nimpongeze kwa kuwapigania sana watu wa Kilolo kuhusu hii barabara, sasa majibu yangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema kwamba Waziri wa Fedha amesha saini mkataba huu na labda tu nielezee kwamba mkataba huu unafadhiliwa na Benki ya Dunia ambao umechukua muda kutokana na ukweli kwamba mradi huu ulikuwa una cover mikoa michache, kwa hiyo Serikali iliona huu mradi utanuliwe, pia ulikuwa unalenga sana barabara za changarawe, kwa hiyo, Serikali ikaona hatuwezi tukachukua fedha World Bank kwa ajili ya changarawe, kwa hiyo, kukawa na majadiliano ili kuuboresha, kwanza uchukue mikoa mingi pia uwe ni kwa kiwango cha lami ambapo ni barabara za kutoka vijijini kuunganisha na barabara za mikoa na barabara kuu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo baada ya kusaini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii kilometa zote 33 zipo kwenye mpango, na zitajengwa ndio maana tunafanya design upya kuhuisha ile design iliyokuwepo ili iendani na kiwango cha sasa cha barabara.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, mimi Mheshimiwa Mbunge nimhakikishie kwamba nipo tayari kuambatana naye kwa ajili ya kwenda kuangalia hizi barabara na kuhakiki jinsi ujenzi unavyoendelea, ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Iringa Mjini hadi Kilolo ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, na mimi kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Iko barabara ya kiuchumi barabara ya ukombozi kwa Wilaya ya Liwale, barabara ya Nangurukuru - Liwale. Barabara hii bajeti ya mwaka jana ilitengewa fedha kwa ajili ya kufanyiwa upembuzi yakini na usanifu wa kina, na mwaka huu pia imetengwa kwenye kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Wana Liwale wangetaka kusikia, ni lini barabara hii itakwisha kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, na hatimaye kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti tuliyopanga, tunauhakikia tutakamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara yote, lakini pia katika maeneo yale kofofi, tumemuagazi Meneja wa TANROADS ayape kipaumbele ili kuhakikisha kwamba yanatengenezwa vizuri ili yasiathiri kupita kipindi kile cha masika, ahsante.