Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 60 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 503 2021-06-28

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Iringa Mjini hadi Kilolo ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Justin Lazaro Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Iringa Mjini hadi Kilolo yenye urefu wa kilometa 33.6 ni sehemu ya barabara ya Iringa iliyoanzia Ipogolo – Idete yenye urefu wa kilometa 67.7 ambayo ni barabara ya Mkoa inayosimamiwa na Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara nchini (TANROADS). Kilometa 9.9 za barabara hiyo ni za lami na kilometa 23.7 nyingine ni za changarawe.

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa barabara ya Iringa Mjini hadi Kilolo, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) ilikamilisha Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hiyo mwaka 2009. Kwa sasa ujenzi wa kilometa 10 kwa kiwango cha lami kati ya kilometa 23.7 za changarawe unaendelea huku marejeo ya usanifu wa mwaka 2009 yakiendelea.

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu itaendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami wa kilometa 13.7 zilizosalia kadri ya upatikanaji wa fedha. Aidha, Serikali itaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara yote kutoka Iringa Mjini hadi Idete kuhakikisha kuwa inapitika vipindi vyote vya mwaka, ahsante.