Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA PARESSO K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege Tanga aliyoitoa Mheshimiwa Rais wakati wa uzinduzi wa Bomba la Mafuta pale Chongoleni Mkoani Tanga itaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimwa Spika, ahsante, kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimwa Spika, kwa kuwa fursa kama hizi mfano Ujenzi wa Mradi wa Bomba la Gesi ni fursa nzuri sana kiuchumi katika nchi na kwa kuwa Serikali imesema italipa fidia kwa ajili ya upanuzi wa uwanja huo wa Tanga, lakini je, Serikali haioni ipo haja ya dharura hata kutafuta mkopo wa dharura ili fursa hii ya ujenzi wa bomba la gesi uendane na ukarabati wa uwanja huo wa Tanga?

Mheshimwa Spika, swali la pili, kuna mchakato pia wa upanuzi wa uwanja wa Lake Manyara, Karatu ambao ni uwanja muhimu sana kwa utalii katika Kanda ya Ngorongoro – Serengeti, wananchi wale hawajalipwa fidia muda mrefu.

Je, ni lini sasa Serikali italipa fidia wananchi hawa wa Lake Manyara pale Karatu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza naamini anakusudia kusema bomba la mafuta na si bomba la gesi; kama hivyo ndivyo Serikali inatambua umuhimu wa bomba hili na ndio maana tunapoongea hivi tayari kuna watu wanafanya tathimini kwa ajili ya watu watakaopisha upanuzi wa kiwanja hiki ili uwanja huu uendane na kasi ya utekelezaji wa mradi wa bomba la mafuta la kutoka Tanga kwenda Uganda. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali inalitambua hivyo na ndio maana iko kasi kuhakikisha kwamba uwanja huu unajengwa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kama amesikiliza kwenye jibu langu la msingi nimetaja viwanja 11 ambavyo viko katika mpango huu na katika kitabu chetu cha bajeti ambayo imepitishwa kiwanja cha Lake Manyara ni kati ya viwanja hivyo 11 ambavyo pia vinafanyika upembuzi yakinifu na usanifu wa kina unafanyika hili kuweza kuhakikisha kwamba ndege sasa zinatua uwanja huu wa Lake Manyara kwa ajili ya kuongeza shughuli za utalii eneo hili la Mkoa wa Manyara na Karatu kwa ujumla wake, ahsante.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. CECILIA PARESSO K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege Tanga aliyoitoa Mheshimiwa Rais wakati wa uzinduzi wa Bomba la Mafuta pale Chongoleni Mkoani Tanga itaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, mimi nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, hii barabara inayotoka Klabu ya Yanga inapita Kata ya Jangwani na Mchikichini na kuja kuunganisha kwenye barabara ya Kawawa ni barabara ambayo inachukua magari takribani 40,000 kwa siku na hali ya barabara hii ni mbaya, haipitiki, inaleta msongamano na kero kubwa sana kwa watumiaji wa barabara hii.

Je Serikali imechukuwa hatua gani kuboresha barabara hii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zungu Mbunge wa Ilala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hizi alizozitaja Mheshimiwa Zungu katika moja ya vikao alitoa kama Mwenyekiti na nimempa taarifa kwamba baada ya kulisemea hilo TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam wako site kuangalia barabara hii ili waweze kuikarabati na kuondoa mashimo yote ili changamoto ambaza zinatokea ziweze kuondolewa.

Kwa hiyo, ni mhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuliahidi kwamba tutalifanyia kazi tumeshalifanyia kazi na TANROADS Dar es Salaam wako site kuhakikisha kwamba changamoto ambayo ipo kwenye hizi barabara inatatuliwa haraka, ahsante.