Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 59 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 493 2021-06-25

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA PARESSO K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: -

Je, ni lini ahadi ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege Tanga aliyoitoa Mheshimiwa Rais wakati wa uzinduzi wa Bomba la Mafuta pale Chongoleni Mkoani Tanga itaanza kutekelezwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Mwanaisha Ng’azi Ulenge, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kiwanja cha Ndege cha Tanga ni miongoni mwa viwanja 11 vya ndege vinavyofanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ufadhili wa Benki ya Dunia kupitia Transport Sector Support Project.

Mheshimwa Spika, Benki ya Dunia imeonesha nia ya kufadhili upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Tanga kupitia programu iitwayo Development Corridor Transport Programme.

Mheshimwa Spika, kwa sasa majadiliano kati ya Serikali na Benki ya Dunia kuhusu malipo ya fidia kwa wananchi watakaopisha utekelezaji wa mradi wa upanuzi na ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Tanga, mapitio ya awali ya ripoti ya mradi huu pamoja na maandalizi ya taarifa mbalimbali zinazohitajika kabla ya mkataba wa mkopo kusainiwa yanaendelea.

Mheshimwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Engineer Mwanaisha Ng’azi Ulenge kuwa Serikali ina nia ya dhati ya kufanya upanuzi na ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Tanga. Aidha, majadiliano kati ya Serikali na Benki ya Dunia yatakapokamilika utekelezaji wa mradi huu utaanza mara moja. Ahsante.