Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, ni lini Mamlaka ya Mji Mdogo Nansio itatambuliwa rasmi na kuanza kuwahudumia wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru na nishukuru kwa majibu ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, ni kweli TAMISEMI walituma timu ikaja kufanya mapitio lakini tokea wakati ule tayari vile vigezo vyote viwili vilivyoonekana havijafikiwa kwa maana ya idadi ya kata ziko kata 12 na idadi ya watu ambacho ni kigezo namba mbili tayari mamlaka ile ina watu zaidi ya 200,000 ni zaidi ya kigezo ilichowekwa na Serikali.

Mheshimiwa Spika, swali langu sasa, je, Serikali kupitia Ofisi ya Rais - TAMISEMI, wako tayari sasa kuridhia kuifanya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Nansio kuwa halmashauri ya mjini? Nashukuru sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA SERIKALI ZA MITAA (DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mkundi, Mbunge wa Ukerewe kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye swali la msingi kwamba kwa wakati huo wakati tadhimini inafanyika Nansio ilikuwa haijafikia vigezo vilivyokuwa vinahitajika, lakini kwa taarifa ya Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa tumeshafikia vigezo hivyo naomba tulichukue jambo hili kama Serikali tukalifanyie tathimini, lakini pia tukajiridhishe kama vigezo hivyo vimefikiwa ndipo tuweze kuona hatua zinazofuata kwa ajili ya kufanya maamuzi. Nakushukuru.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, ni lini Mamlaka ya Mji Mdogo Nansio itatambuliwa rasmi na kuanza kuwahudumia wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuwa Mji Mdogo wa Namanyere tulishakidhi vigezo na taarifa ziko ofisini kwenu; ni lini sasa mtachukua hatua kwa mujibu wa sheria ili na sisi tuweze kupata Halmashauri ya Mji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana na kwa niaba ya Waziri Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kimsingi taratibu za kupandisha Mamlaka za Miji Midogo kwenda kuwa Halmashauri za Miji zina utaratibu wake, lakini zina sheria yake na hivyo Serikali siku zote inafanya tathimini kuona kama vigezo vimefikiwa na baada ya hapo hatua stahiki zinachukuliwa.

Kwa hiyo, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwa taarifa aliyoitoa Serikali pia tutakwenda kupitia vigezo vya Halmashauri kwa maana ya Mji Mdogo wa Namanyere na kama umekidhi vigezo Serikali itachukua hatua kwa mujibu wa taratibu. Ahsante.