Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa uamuzi wa mwisho wa mapendekezo ya mgawanyo wa rasilimali, madeni, majengo, watumishi na mashamba kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu na Halmashauri ya Mji wa Mbulu?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo ya nyongeza. Kwa kuwa mgawanyo huu ulifanyika mwaka 2015/2016, ni miaka mitano, sita sasa; na kwa kuwa hadi sasa hakuna tamko la wazi la Wizara kuwasilishwa mbele ya Mabaraza ya Madiwani wa Halmashauri zote mbili ili kuondoa hali ya madeni mbalimbali na rasilimali nyingine na mkanganyiko uliopo: -

Je, ni lini sasa Wizara itawasilisha mgawanyo huu kwa waraka maalum wenye GN mbele ya Mabaraza hayo mawili? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa katika mgawanyo wa rasilimali tulizopokea ni pamoja na watumishi; Halmashauri ya Mji Mbulu sasa inakabiliwa na upungufu mkubwa sana wa watumishi takribani miaka sita sasa kwa ajili ya hizo asilimia 40 ambapo wengine wamestaafu na wengine wamefariki kwa sababu mbalimbali: -

Je, lini sasa Serikali itaondoa tatizo hili la upungufu wa watumishi hawa angalau kwa awamu katika sekta mbalimbali katika Halmashauri yetu ya Mji wa Mbulu? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mheshimiwa Zacharia Paul Issaay katika swali lake la kwanza alikuwa tu anataka kwamba kujua ni lini Serikali itatoa tamko la wazi ambalo litawasilishwa katika mabaraza ili kutoa waraka maalum ili hizi Halmashauri mbili ziweze kujua sasa zimeshagawanyika rasmi.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu, kwa sababu jambo hili limefanyika muda mrefu, ninaiagiza Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwamba waandike hili tamko la wazi haraka iwezekanavyo na ndani ya miezi mitatu jukumu hilo tutakuwa tumeshalifanya na mabaraza hayo mawili yatakuwa yamekaa ili wawe wanajua kabisa rasmi wameshaganyika. Kwa hiyo, ndani ya miezi mitatu tutakuwa tumeshalitekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, ni kero ya watumishi wachache katika eneo lake na anataka kujua Serikali itatatua lini tatizo hili; niseme tu Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, tutashirikiana kwa Pamoja, kwa sababu wanaotoa kibali cha kuajiri watumishi ni Ofisi ya Raisi Utumishi na Utawala Bora na sisi jukumu letu ni kupata hao watumishi na kuwapangia vituo na maeneo ya kwenda kufanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, wale ambao tunaendelea kuwajiri kama ambavyo tumekuwa tukiendelea kuajiri walimu, tumekuwa tukiendela kuajiri watumishi katika kada ya afya, tunaendelea kuwaleta katika Halmashauri zetu nchi kwa kadri tutakavyokuwa tunapata kulingana na kibali tunavyopewa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Kwa hiyo, niseme tu kwamba Mheshimiwa Mbunge tutaendelea kuleta watumishi katika eneo lako kwa kadri tutakavyokuwa tunapewa kibali na bajeti ya Serikali inavyohitaji. Ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa uamuzi wa mwisho wa mapendekezo ya mgawanyo wa rasilimali, madeni, majengo, watumishi na mashamba kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu na Halmashauri ya Mji wa Mbulu?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa
kuwa mgawanyo wa Halmashauri hizi mbili ulitangazwa kwenye GN ya mwaka 2015, kwa nini sasa ichukuwe miezi mitatu wakati tangazo liko wazi na sheria hii iko wazi sana?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Flatei Massay ameeleza kwamba GN ni kweli ilitoka mwaka 2015 lakini bahati mbaya sana tamko la wazi lilicheleweshwa kuwasilishwa. Kwa hiyo, nikiri kabisa kwamba nafikiri kulikuwa na kupitiwa kwenye utekelezaji wa jambo hili na ndiyo maana, kwa sababu Serikali ya Awamu ya Sita tuko hapa, tumeahidi kulitekeleza ndani ya miezi mitatu ili kuhakikisha jambo hili limeisha kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa uamuzi wa mwisho wa mapendekezo ya mgawanyo wa rasilimali, madeni, majengo, watumishi na mashamba kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu na Halmashauri ya Mji wa Mbulu?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa mgawanyo wa mali iliyokuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam haukuhusisha wadau wakiwepo Waheshimiwa Wabunge: -

Je, Serikali haioni sasa haja ya kuu-review ule mgao hasa katika ile mikopo ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu?

NAIBU SPIKA: Nataka kuamini ukisema Wabunge, unamaanisha pia na Madiwani hawakushirikishwa. Kwa sababu kama walishirikishwa Madiwani halafu Wabunge ndio hamkuwepo, ni ninyi ambao hamkuwepo. Hebu fafanua kidogo.

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mabaraza ya Madiwani wa Halmashauri za Jiji la Dar es Salaam hayakushirikishwa.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Jambo alilolita Mheshimiwa Abdallah Chaurembo ni kubwa sana ambalo linahitaji kwanza tufuatilie, tujiridhishe kwa sababu ninaamini kila jambo linapofanyika kunakuwa na muhtasari ambao huwa unaandikwa na vikao na idadi ya watu waliohudhuria.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, endapo jambo hilo halikufanyika, basi ninaamini Ofisi ya Rais, TAMISEMI itazingatia namna bora kabisa ambayo itasaidia jambo hili liweze kufanyika kikamilifu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunalipokea na tutakwenda kulifanyia kazi, ahsante sana.