Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 58 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 488 2021-06-24

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa uamuzi wa mwisho wa mapendekezo ya mgawanyo wa rasilimali, madeni, majengo, watumishi na mashamba kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu na Halmashauri ya Mji wa Mbulu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu katika swali Na. 116 tarehe 12 Januari, 2021 mgawanyo wa rasilimali watu, magari, pikipiki, rasilimali na madeni kati ya Halmashauri ya Mji Mbulu na Halmashauri ya Mbulu umefanyika kwa asilimia
100 kwa kuzingatia mwongozo wa ugawaji wa mali na madeni ulioandaliwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI wa Mwaka
2014. Katika mgawanyo huo Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu kwa maana ya Halmashauri mama, ilipata asilimia 60 na Halmashauri ya Mji wa Mbulu ilipata asilimia 40.