Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mkwiti – Amkeni inayounganisha Mkoa wa Lindi na Mtwara kupitia Mtama?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante barabara ya kutoka Amkeni – Kitangali hadi Mtama yenye kilomita 74 ndiyo barabara pekee inayofungua mji wa Newala na maeneo mengine kuelekea Dar es Salaam hadi kuja huku Dodoma. Nakubaliana na Mheshimiwa Waziri kwamba fedha zitatengwa kwa awamu lakini ikumbukwe kwamba wilaya hii ni ya muda mrefu tangu 1952 hadi leo haina barabara ya uhakika. Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kutosha ili barabara hii iweze kukamilika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kutokana na changamoto za ubovu wa hii barabara wafanyabiashara wengi wa usafirishaji wanakwama kupeleka vyombo vyao vya usafiri kwa hofu ya uharibifu wa vyombo vyao na wananchi wanateseka na usafiri kwa sababu ya ubovu wa barabara. Je, Serikali haioni kwamba inarudisha nyuma jitihada zake za ajira kupitia sekta zisizo rasmi hasa usafirishaji? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge wa Newala Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi barabara hii ni kweli ni ya muhimu sana kwa mkoa wa Mtwara ambayo inaunganisha mkoa wa Lindi. Lakini kwa kulitambua hilo Wizara ya Ujenzi kupitia TANROAD inajenga maeneo korofi yote kwa kiwango cha lami na Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba maeneo mengi korofi yamejengwa kwa kiwango cha lami na hata katika mwaka huu wa fedha tunaoendea kuna fedha imetengwa kwa ajili ya kujenga kwa kiwango cha lami yale maeneo yote korofi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la pili, ambalo linafanana hili jibu la kwanza kwa sababu ya kutambua ule ubovu kwenye hii barabara ndiyo maana sasa TANROADS Mkoa wa Mtwara unafanya kila jitihada kuhakikisha kwamba barabara hii inapitika muda wote na kuhakikisha kwamba maeneo korofi yote yanawekewa lami ili barabara hii iweze kupitika muda wote wa mwaka ahsante.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mkwiti – Amkeni inayounganisha Mkoa wa Lindi na Mtwara kupitia Mtama?

Supplementary Question 2

MHE. NAGHENJWA L KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa katika mwaka wa fedha huu 2021 Serikali ilisema imetenga bilioni 5 kwa ajili ya kujenga barabara ya kutoka Same Kisiwani mpaka Mkomazi kwa kiwango cha lami. Je, fedha hiyo itatolewa lini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kaboyoka Viti Maalum kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema fedha hii kwa kujenga kwa kuanza kwa kiwango cha lami Same hadi Mkomazi ambapo tumetenga bilioni 5 fedha itaanza kutoka mara bajeti itakapoanza kutumika ya mwaka 2021/2022, ahsante.

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mkwiti – Amkeni inayounganisha Mkoa wa Lindi na Mtwara kupitia Mtama?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa kuwa barabara hii ya Mkwiti – Amkeni inayounganisha mkoa wa Lindi na Mtwara tatizo lake linafanana kabisa na barabara ya Singida Simiyu inayoanzia Iguguno na kwa kuwa Serikali imevunja nyumba za wananchi wa Iguguno hivi karibuni.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi barabara hii hasa kuanzia Iguguno mpaka Nduguti?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja ni barabara ambazo zitajengwa katika kipindi hiki cha miaka mitano na itategemea na upatikanaji wa fedha hatuwezi leo tukaahidi kwamba itaanza mwaka ujao kwa sababu haijaingia kwenye mpango. Lakini nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika miaka inayokuja ya bajeti itaingizwa kwenye mpango ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami ikiwa ni kuanzia na upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na hatimaye kujenga kwa kiwango cha lami ahsante.

Name

Christopher Olonyokie Ole-Sendeka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mkwiti – Amkeni inayounganisha Mkoa wa Lindi na Mtwara kupitia Mtama?

Supplementary Question 4

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa kuwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara inayotoka Arusha, Simanjiro, Kiteto, Kongwa umekamilika na ni ahadi ya muda mrefu ya ilani za uchaguzi kadhaa. Je, ni lini Serikali Sikivu ya CCM itaanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidiwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sendeka Mbunge wa Simanjiro kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii aliyoitaja ni barabara muhimu sana hasa kwa mikoa ya Arusha Manyara na Dodoma na nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kati ya barabara ambazo ziko kwenye mpango na kwa kuwa usanifu umeshakamilika Serikali inatafuta fedha ili barabara hii ianze kujengwa kwa kiwango cha lami katika awamu ambayo ime...

MWENYEKITI: Ahsante ameshakuelewa barabara inajengwa Mheshimiwa Naibu Waziri.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mkwiti – Amkeni inayounganisha Mkoa wa Lindi na Mtwara kupitia Mtama?

Supplementary Question 5

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuwa barabara ya kutoka Busisi Nyang’wale kwenda Kahama imeahidiwa na viongozi wakuu wa nchi kujengwa kwa kiwango cha lami. Ni lini Serikali itaanza upembuzi yakinifu na ujenzi wa barabara hiyo kuanza mara moja?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amar Mbunge wa Nyang’wale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni barabara ambayo katika ilani ya chama itafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika kipindi hiki. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge avute Subira fedha ikipatikana ya Serikali tutafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na kama fedha itaruhusu basi tutaanza kuijenga kwa kiwango cha lami ahsante.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mkwiti – Amkeni inayounganisha Mkoa wa Lindi na Mtwara kupitia Mtama?

Supplementary Question 6

MHE. PHILIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, swali langu la nyongeza, barabara ya kutoka Mbalizi mpaka Mkwajuni sasa ni miaka 15 imekuwa ikiahidiwa na Waheshimiwa Marais wanaokuja kupiga kampeni kule Mheshimiwa Dkt. Kikwete alituahidi miaka 10 ikapita bila kujenga, Mheshimiwa Rais marehemu Mungu amlaze mahali pema peponi Mheshimiwa JPM naye aliahidi…

MWENYEKITI: Usilete ufundi kwenye swali uliza swali moja kwa moja. (Kicheko)

MHE. PHILIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Waziri ni lini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami kutoka Mbalizi mpaka Mkwajuni kwa sababu nimekuwa nikiahidiwa miaka mingi? Na upembuzi yakinifu tayari umeshaisha kabisa naomba majibu.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Phillipo Mulugo Mbunge wa Songwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikubaliane kwamba barabara hii ni muhimu sana kwa Mkoa wa Songwe lakini pia kwa wilaya ya Chunya na wilaya ya Songwe. Barabara hii imeahidiwa kujengwa kwa kiwango cha lami lakini bado nimpe pole sana Mheshimiwa kwa sababu katika kipindi chote hiki ilikuwa haipitiki kwa sababu ya mvua lakini TANROADS mkoa wa Songwe ilifanya jitihada kuhakikisha kwamba barabara hii inapitika. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mulugo kwamba katika kipindi hiki cha miaka mitano kama ilivyoahidiwa na tunavyotekeleza ilani za viongozi wakuu wa Serikali barabara hii nayo itafanyiwa kazi kwa maana ya kujengwa kwa kiwango cha lami kadri fedha itakavyopatikana, ahsante.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mkwiti – Amkeni inayounganisha Mkoa wa Lindi na Mtwara kupitia Mtama?

Supplementary Question 7

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi barabara ya Mafinga Mgololo ambayo ni kiungo muhimu sana cha uchumi katika uchumi wa Mufindi na Iringa imeahidiwa toka ilani ya uchaguzi 2005 ninauliza Serikali. Je, wakati jitihada za kujenga kwa kiwango cha lami zinaendelea Serikali iko tayari kushughulikia na maeneo korofi kama vile Itulavanu, Mtili na pale mlima wa Kalinga?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chami Mbunge wa Mafinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kupitia Bunge hili nimuagize Meneja wa TANROADS Mkoa wa Iringa aende akaangalie maeneo hayo korofi aweze kufanya tathmini ili yale maeneo korofi tuweze kutafuta fedha ili barabara hiyo iweze kutengenezwa maeneo korofi yaweze kupitika muda wote wa mwaka. Ahsante.