Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 57 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 484 2021-06-23

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mkwiti – Amkeni inayounganisha Mkoa wa Lindi na Mtwara kupitia Mtama?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge wa Newala Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mkwiti – Amkeni yenye urefu wa kilometa 74.23 inayounganisha Wilaya ya Tandahimba na Newala katika Mkoa wa Mtwara na Wilaya ya Lindi Vijijini mkoa wa Lindi unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Katika mwaka wa fedha 2020/2021, jumla ya shilingi milioni 1,807.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami wa kilometa tatu ambapo jumla ya kilometa 2.8 zimekamilika kujengwa na kazi za ujenzi zinaendelea kwenye kipande chenye urefu wa mita 200. Wakati ujenzi kwa kiwango cha lami ukiendelea kutekelezwa kwa awamu, Wizara yangu itaendelea kuifanyia matengenezo barabara hiyo ili iweze kupitika majira yote ahsante.