Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa umeme wa Grid ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Stephen Byabato, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwanza tunaishukuru Serikali kwa mradi. Swali la kwanza; Kata za Kasansa, Mamba, Maji Moto, Mbede Mwamapuli, Chamalendi, Usevya na Kibaoni zinatumia umeme wa kutoka nchi ya jirani ya Zambia, umeme ambao hautoshi ni kilowatt 100. Tuliomba kupata umeme wenye kilowatt 500. Je ni lini Serikali itatuletea transformer zenye kilowatt 500?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwenye Mji ya Nyonga ambao ni Makao Makuu ya Wilaya ya Mlele umeme hautoshi kwa sababu umeme uliopo wakati unawekwa ulikuwa umewekwa kwa mahitaji madogo, mji umeongezeka, wananchi wanafanya biashara, wamefungua miradi ya ujasiriamali, ambayo ni mashine za kusaga na vitu vingine. Je, Serikali haioni umuhimu wa kutuongezea umeme wenye megawatt zaidi ya nne?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Taska Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum kwa pamoja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru kwa kutambua juhudi za Serikali za kuhakikisha kwamba gridi ya Taifa inafika katika Mkoa wetu wa Katavi. Mkoa wa Katavi haujafikiwa na gridi lakini unapata umeme kutoka katika vyanzo viwili, Wilaya ya Tanganyika na Wilaya ya Mpanda Mjini wanatumia generator mbili ambazo ziko pale Mpanda mjini na mpaka sasa zinazalisha megawatt kama 5.87 hivi na umeme ule unatosha maeneo yale kwa sababu matumizi ya Mkoa wa Katavi kwa sasa kwenye yale maeneo ya mjini ni megawatt kama 5.2.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini chanzo cha pili cha umeme kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge ni umeme ule unaotoka Zambia unapita Sumbawanga unapita Namanyere unakuja kuingia sehemu ya karibu na Mpanda Mjini unakuja kuingia kwenye Wilaya ya Mlele kwenye hayo maeneo ya Mwamapuli, Maeneo ya Majimoto, Maeneo ya Kibaoni aliyoyataja ambayo sasa ndio umeme unaingia pale kutokea Sumbawanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inachokifanya kwa sasa cha kwanza kabisa inahakikisha kufikia 2023 imefikisha gridi ya Taifa katika Mkoa wetu wa Mpanda kutokea Tabora. Jambo la pili ambalo inalifanya ni kuhakikisha kwamba inaongeza uwezo wa hizo transformer.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wiki iliyopita transformer yenye uwezo wa kilowatt 400 imeongezwa katika Wilaya ya Mlele ili kuongeza nguvu kwenye hayo maeneo ya Kata za Mlele ambazo amezitaja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Mheshimiwa Mbunge afanye mawasiliano, atataarifiwa kwamba sasa hali ya umeme imetulia na sasa Katavi inaweza kuendelea vizuri wakati tukiwa tunahakikisha kwamba gridi inafika kwenye Mkoa wetu wa Katavi.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa umeme wa Grid ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Wilaya ya Tanganyika ni miongoni mwa Wilaya ambazo zilichelewa sana kupata umeme wa REA. Kwa bahati nzuri kwa sasa Serikali inatekeleza mradi huo. Kwenye Mradi wa REA phase II vipo vijiji vilisahaulika kuingizwa kwenye mradi. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha vijiji vilivyosahaulika katika mradi wa phase II?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakoso, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri katika swali la msingi na swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Mbogo. Pia nimpongeze sana Mheshimiwa Kakoso pamoja na Waheshimiwa Wabunge wote wa Katavi pamoja na Mpanda wanavyofuatilia masuala ya umeme vijijini katika maeneo yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli yapo maeneo nchi nzima ambayo yalisahaulika na yalikuwa yanafikia takriban maeneo ama vijiji 610.

Napenda kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge pamoja na Mheshimiwa Kakoso vijiji vyote 610 ambavyo vilisahaulika tumefanya marejeo na vijiji vyote vimeingia kwenye mpango na vimekabidhiwa wakandarasi kwa ajili ya utekelezaji wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Kakoso kwa sababu ni kweli hata kata kubwa ya Mishamo pamoja na Mwese pamoja na Utamata vilisahaulika lakini vyote vimeingia kwenye mpango na wananchi wote watapata umeme kwa uhakika ndani ya miezi 18 kutoka sasa. (Makofi)

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa umeme wa Grid ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 3

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuuliza, je, ni lini Serikali itaweza kutuongezea transformer nyingine kwenye Jimbo la Temeke kwani tuna mahitaji ya megawatt 117, lakini sasa hivi tunatumia megawatt 32. Je, tutapata lini transformer hii nyingine? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilave, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Jimbo la Temeke pamoja na Mbagala na Mkuranga tumelazimika kuongeza vituo vitatu katika kila wilaya kwa ajili ya kuongeza transformer za megawatt 48 kila mahali, kwa hiyo Temeke, Mbagala pamoja na Mkuranga tunaongezea transformer ya megawatt 48 kila eneo. (Makofi)

Name

Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa umeme wa Grid ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 4

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia swali dogo la nyongeza. Wilaya ya Shinyanga Mjini licha ya kuwepo kwa umeme wa kutosha kutoka kwenye gridi ya Taifa, lakini kumekuwa na tatizo kubwa sana la kukatikakatika kwa umeme. Je, Serikali ipo tayari sasa kuja na hasa Mheshimiwa Naibu Waziri, yupo tayari kuongozana na mimi kwenda kule Shinyanga Mjini kusikiliza wananchi jinsi wanavyoathirika kibiashara pamoja na kijamii?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mayenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namruhusu Mheshimiwa Naibu Waziri kufuatana naye katika Jimbo lake kwa siku alizotaja. Hata hivyo, tatizo la kukatika kwa umeme katika Mkoa wa Shinyanga inatokana na matengenezo yanayofanyika kwa sasa katika line ya Segese ya umbali wa kilometa 12. Kwa hiyo mara nyingi tunataoa matangazo kurejesha hali ya umeme katika hali yake ya kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Shinyanga unapata umeme kutoka substation ya Ibadakuli yenye megawatt 182 ambapo mahitaji ya Mkoa wa Shinyanga ni Megawatt 123. Kwa hiyo umeme wa Mkoa wa Shinyanga unatosha, isipokuwa kwa sasa wananchi tunaomba radhi katika maeneo yote yanayopitiwa ikiwemo Ngokoro na maeneo mengine kwa sababu ya matengenezo ya line ya Segese. Ndani ya 14 matengenezo yatakamilika na umeme utarejea katika hali yake ya kawaida.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa umeme wa Grid ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 5

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Njombe tunapitiwa na gridi inayotoka Makambako kwenda Songea, lakini bado tumekuwa na tatizo kubwa sana la ukatikaji wa umeme ambao sisi tunaamini pamoja na maelezo ambayo Waziri ameyatoa siku ya nyuma, tunaamini kutokana na grid stability, ni lini sasa suala la ukatikaji wa umeme usioisha wa Mkoa wa Njombe na Mji ya Njombe utafikia tamati? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwanyika, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hasa katika eneo la Njombe pamoja na Ludewa umeme unakatika kwa kiasi kikubwa kwa sababu kuna matengenezo ya kufunga auto recloser ambayo inaimarika ndani ya siku 28. Pia katika maeneo ya Njombe na Ludewa ipo line ambayo tunaongezea, tumetenga shilingi bilioni 270 katika mikoa miwili na bilioni 100 kila mkoa kwa ajili ya shughuli za ukarabati wa mitambo na kuimarisha umeme katika Mkoa wa Makambako, Njombe pamoja na Ludewa. Kwa hiyo niwahakikishie wananchi wa Ludewa pamoja na Njombe kwamba ndani ya muda unaokuja ambao nimeutaja hali ya umeme itaimarika kwa kiasi kikubwa.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa umeme wa Grid ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 6

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini ilitupa orodha ya makandarasi ambao wanafanya kazi katika wilaya zetu na majimbo yetu. Sasa, je, Serikali inaweza ikatupatia orodha ya awamu hii ya REA ya tatu, mzunguko wa pili, ni vijiji vipi na vitongoji vipi vitakavyofanyiwa kazi ili iwe rahisi kwa Waheshimiwa Wabunge kufuatilia na kutoa taarifa Serikalini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipotoa yale mawasiliano ya mkandarasi na baadaye tukatoa mawasiliano ya Mbunge kwa Mkandarasi, tuliamini kwamba kwenye mawasiliano hayo masuala yote yanayohusiana na upelekaji wa umeme kwenye maeneo yetu yatafanyika. Aidha, sisi kama Wizara tuko tayari kuendelea kutoa ushirikiano na kutoa taarifa sahihi kabisa na kubwa kabisa za maeneo yapi yatakayofikiwa na umeme ili Waheshimiwa Wabunge sasa watuambie yale ambayo yanaonekana yamebaki kama Mheshimiwa Waziri alivyosema, vile vijiji 600 tayari tumevichukua ili sasa kwa wigo mpana tuweze kushirikiana pamoja kuhakikisha maeneo yote yanachukuliwa.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa umeme wa Grid ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 7

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa majimbo ya mijini mitaa ndio kama vijiji. Swali, je, ni lini sasa Serikali itapeleka umeme kwenye mitaa yetu kwa mfano Jimbo la Iringa Mjini kata ya Isakalilo, Mtaa wa Kitasengwa Mkonga, Majengo Mapya; Kata ya Mkwawa, Mtaa wa Wahe na Hoho, Kata ya Igumbilo Mtaa wa Ulongeā€¦

MWENYEKITI: Sio zote tena wewe taja moja tu.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia umeme katika mitaa. Sasa naomba nijibu swali lake la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tumetenga mitaa 637 kwa nchi nzima ikiwemo mitaa kwa Mheshimiwa Jesca na mitaa yote itaanza kupelekewa umeme kuanzia mwezi Novemba mwaka huu ndani ya miezi 18. Tumetenga fedha hizo kwa awamu tunaanza na mitaa yote ambayo inafanana na hali ya kivijiji, lakini na mitaa mingine ambayo ipo katika majiji makubwa pamoja na manispaa kwa nchi nzima. Ahsante sana. (Makofi)