Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 57 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 482 2021-06-23

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa umeme wa Grid ya Taifa Mkoani Katavi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Njia Kuu ya Kusafirisha Umeme wa Gridi ya Taifa wa msongo wa kilovolti 132, yenye urefu wa kilometa 381 kutoka Tabora hadi Katavi. Mradi huu unahusisha pia ujenzi wa vituo vitatu vya kupoza umeme vya msongo wa kilovoti 132 kwenda 33 vya Ipole, Inyonga na Mpanda. Ujenzi wa Mradi unatarajia kukamilika ifikapo mwezi Agosti, 2023. Gharama ya mradi ni Shilingi Bilioni 64.5.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa mradi mwingine wa njia ya kusafirisha umeme mkubwa wa kilovoti 400 kutoka Iringa - Mbeya – Sumbawanga – Mpanda hadi Kigoma yenye urefu wa kilometa 1,232, unatarajiwa kuanza Novemba na kukamilika mwezi Oktoba, 2024. Gharama ya mradi ni Shilingi Bilioni 470.42.