Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Mamlaka ya Mji Mdogo wa Namanyere imetimiza vigezo vyote vya kuwa Halmashauri ya Mji. Je, ni lini Serikali itaipa hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji Mamlaka hiyo ya Mji mdogo wa Namanyere?

Supplementary Question 1

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Tunaposukuma uanzishwaji wa mamlaka hizi, tunataka kuharakisha maendeleo kwa wananchi. Mji wa Namanyere umekuwa na maombi haya muda mrefu na majibu yamekuwa ya namna hii hii, tangu Bunge lililopita majibu yamekuwa ni haya ya kusema kuna timu ya wataalam watakwenda kuhakiki ili majibu ya kuanzisha yapatikane. Nataka kujua kama Serikali inaweza ikatoa hasa tarehe maalum au time frame ili wananchi wajue hasa ni lini zoezi hili litakamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, miji midogo mingi hapa nchini inaendelea kukuwa ikiwepo ile ya Chala, Kate ambako ni Makao Makuu ya Jimbo, Wampembe, Kipande na kwingineko, lakini mpangilio wake umekuwa si mzuri sana kutokana na Halmashauri kukosa fedha za kufanya utaratibu wa mipango ya uendelezaji wa miji hiyo. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya ukuaji huu wa miji usioridhisha hapa nchini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mipata, anataka time frame ya lini jambo hili litakamilika. Mheshimiwa Mipata amekuja ofisini kwangu si chini ya mara mbili katika jambo hili na siyo Mipata peke yake na wadau mbalimbali wengine kutoka Lushoto, wengine kutoka maeneo mbalimbali kwa ajili ya jambo hili. Ndiyo maana nilisema hapa siku zilizopita kwamba, jambo hili kwa sababu limekuwa ni kilio cha Wabunge wengi, mpaka Waziri wangu akaagiza kwamba tulete database ya status ya kila maombi haya yamefikia wapi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nieleze, naweza nika-table hii status ya database mpaka kwa kaka yangu pale Ilula, mpaka kwa kaka yangu Profesa Majimarefu wote maombi yao yapo katika hili na hii chati yote iko hapa wataalam wetu tumewaagiza sasa jinsi gani watakwenda kufanya assessment.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili naomba niseme, hapa katikati tumepata matatizo, kuna Halmashauri zingine zinaanzishwa kwa presha hata zile GN namba zinapotajwa zile code zinakosewa, zinapokosewa maana yake unaingilia katika mipaka ya Halmashauri nyingine. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mipata avute subira, sitaki kusema ni lini inaanza, lakini lengo letu kubwa ni kwamba, ndani ya kipindi hiki cha mwaka huu wa fedha tunapoanza, imani yangu kwamba, hii kazi itakwenda kwa kasi kwa sababu hata mimi sipendi kila siku kusimama hapa kujibu swali hilo hilo. Kwa hiyo, imani yangu ni kwamba, jambo hili tutafikia mwisho, wenye kukidhi vigezo watakidhi na wale ambao watakuwa na upungufu wataambiwa wapi warekebishe ili mradi wapate mamlaka. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mipata avute subira.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine alizungumzia suala zima la mipangilio mibaya ya miji. Ni kweli sasa hivi ukiangalia hasa miji mingi inayokua, maeneo mbalimbali yanajengwa kiholela sana. Hata hii miji midogo, kwa mfano, ukienda hata pale Kibaigwa, eneo la karibu tu hapa, ukienda kuna ujenzi kama unatengeneza kachumbari vile, kitunguu, nyanya kila kitu yaani miji imekuwa hovyo hovyo kabisa. Ndiyo maana tunapopita katika Halmashauri zetu tumewaelekeza Maafisa wa Mipango Miji na Maafisa Ardhi, jukumu lao kubwa sio kuchukua mshahara wa Serikali tu na kukaa ofisini, japokuwa resource ni ndogo lakini wakitumia taaluma zao, tutafanikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezekani Afisa Mipango Miji au Afisa Ardhi yuko ofisini pale, nje ya Halmashauri palepale, lakini watu wanaendelea kujenga kiholela katika maeneo yasiyokuwa sawasawa. Tumetoa maelekezo kwamba Maafisa Mipango Miji na Maafisa Ardhi watumie own source zilizokuwepo, kuona jinsi gani watatumia taaluma yao kufanya mipango rafiki ya kijamii, angalau wananchi wetu waishi katika mipango bora. Kwa sababu ukitegemea kwamba utapata bilioni mbili (2) kwa wakati mmoja kupanga mipango miji, inawezekana itakuwa changamoto kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba nimwambie Mheshimiwa Mipata kwamba, tumeliona hili na tumeendelea kutoa maelekezo na kwa kutumia platform hii ya leo naomba niwaagize Maafisa Mipango Miji wote na nilishawaagiza Afisa Mipango Miji wa Bahi na Magu nilikopita kwamba, wahakikishe maeneo yao yote wanapokuwa Ofisini, yanakuwa maeneo rafiki yaliyopangwa vizuri kwa kutumia taaluma zao.

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Mamlaka ya Mji Mdogo wa Namanyere imetimiza vigezo vyote vya kuwa Halmashauri ya Mji. Je, ni lini Serikali itaipa hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji Mamlaka hiyo ya Mji mdogo wa Namanyere?

Supplementary Question 2

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kama ilivyo Mji Mdogo wa Namanyere, katika Wilaya ya Geita kuna Mji Mdogo wa Katoro ambao una hadhi na umetimiza vigezo vyote. Napenda kujua sasa ni lini Mamlaka ya Mji Mdogo huu wa Katoro utapandishwa kuwa Mamlaka ya Mji?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kweli Mji wa Katoro unakua sana hasa katika eneo lile la Mkoa wa Geita. Kutokana na suala la Sekta ya Madini, hali ya miji imekuwa ikikua kwa kasi sana ukiwemo na mji wa Katoro. Kwa hiyo, nipendekeze tu kwa sababu katika database yangu hapa nikiangalia Mji wa Katoro siuoni, kwa hiyo Mheshimiwa Lolesia, kama walishaleta Ofisi ya Rais, TAMISEMI nitakwenda ku-cross check, lakini kama bado hawajaanza huo mchakato, naomba nielekeze sasa jinsi gani tutafanya katika eneo la Halmashauri yao, wahakikishe kwamba wanaanza mchakato wa kawaida kwanza katika Vijiji, katika u-DC, Baraza la Madiwani na baadaye RCC, yale maombi yaje Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutayatathmini, mwisho wa siku ni kwamba, eneo hili litapandishwa kwa vigezo vitakavyokuwa vimefikiwa.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Mamlaka ya Mji Mdogo wa Namanyere imetimiza vigezo vyote vya kuwa Halmashauri ya Mji. Je, ni lini Serikali itaipa hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji Mamlaka hiyo ya Mji mdogo wa Namanyere?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY M. KEISSY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Mheshimiwa Naibu Waziri katika swali lake la kwanza alisema kwamba ana ziara ya Iringa, Mbeya na Songwe. Je, yuko tayari sasa katika hiyo ziara kuunganisha mpaka Wilaya ya Nkasi akajionee mwenyewe matatizo ya Afya, Elimu na Barabara katika Wilaya yetu ya Nkasi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ziara yangu inaanzia Mkoa wa Iringa, nitakwenda Mkoa wa Njombe, Mbeya, Rukwa, nikitoka hapo nitakwenda Mkoa wa Kigoma halafu namalizia Mkoa wa Tabora, hiyo ni phase namba moja. Baadaye nitakwenda Mkoa wa Mara, Geita, Mwanza, Kagera, halafu nitarudia katika Kanda ya Mashariki. Kwa hiyo, Mheshimiwa Keissy mpo katika awamu ya kwanza ya ziara yetu kubaini changamoto ili kuona jinsi gani Ofisi ya Rais TAMISEMI, tutafanya kuwahudumia wananchi wa Tanzania.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Mamlaka ya Mji Mdogo wa Namanyere imetimiza vigezo vyote vya kuwa Halmashauri ya Mji. Je, ni lini Serikali itaipa hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji Mamlaka hiyo ya Mji mdogo wa Namanyere?

Supplementary Question 4

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa hali ya kukamilika kwa vigezo vya kupandisha hadhi miji yetu kule Namanyere iko sawa sawa na kule Maramba ambapo tumetimiza vigezo vya kupata mji mdogo tangu kabla Mkinga haijawa Wilaya. Je, ni lini Mji wa Maramba utapewa hadhi ya kuwa Mji Mdogo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hawa wenzetu walikuwa na maombi yanayogusa sehemu mbili; walikuwa wanaomba hii Maramba iwe mji mdogo, lakini walikuwa wanaomba eneo hili la Mkinga. Naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge, nadhani maombi haya yamepita muda mrefu sana. Sasa nimwombe na nimwagize Mkurugenzi na timu yake kule Halmashauri wakishirikiana naye kwa sababu kulikuwa na maombi haya na muda mrefu sana umepita, waanze huu mchakato vizuri ilimradi itufikie Ofisi ya Rais, TAMISEMI, mwisho wa siku vile vigezo vikiwa vimefikiwa hatutosita kuhakikisha eneo hili linapandishwa hadhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimwagize Mheshimiwa Mbunge na wengine wote, maana yeye ni rafiki yangu tupo humu ndani. Namwambia Mkurugenzi na timu yake yote waanze huu mchakato sasa vizuri ilimradi hili jambo lifike Ofisi ya Rais, TAMISEMI na wataalam wetu waende kuhakiki kwa ajili ya vigezo hivyo