Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 444 2016-06-28

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:-
Mamlaka ya Mji Mdogo wa Namanyere imetimiza vigezo vyote vya kuwa Halmashauri ya Mji.
Je, ni lini Serikali itaipa hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji Mamlaka hiyo ya Mji mdogo wa Namanyere?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Desderius John Mipata, Mbunge wa Nkasi Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, maombi ya kupandishwa hadhi Mamlaka ya Mji mdogo Namanyere kuwa Halmashauri ya Mji yameshapelekwa katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI baada ya kukamilika kwa vikao vya kisheria. Baada ya hatua hiyo, Ofisi ya Rais, TAMISEMI itakwenda kuhakiki vigezo vinavyozingatiwa katika uanzishwaji wa Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira wakati tunakamilisha taratibu za kisheria zinazotakiwa na kufanya uhakiki kabla ya maamuzi ya kuanzisha Halmashauri ya Mji kufikiwa.