Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA K.n.y. MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa barabara ya Njombe – Mdandu – Iyayi kuelekea Mbeya?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza na nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Nina maswali mawili tu ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Kibena Stop Lupembe kutokea Madeke ambayo inaunganisha Mkoa wa Njombe na Morogoro? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; ni lini Serikali itajenga kwa haraka barabara ya Makete ambayo inapita Hifadhi ya Kituro kutokea Mbeya. Sababu barabara zote hizi zina umuhimu kwa Mkoa wetu wa Njombe na zitaongeza uchumi wa Mkoa wa Njombe kwenye masuala ya utalii, lakini vilevile kwenye masuala ya biashara, naomba nipate majibu ya maswali haya. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili kwa pamoja ya Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kibena - Kona kwenda Madeke ambayo inakuja kutokezea Mlimba, Ifakara ni barabara ambayo kwenye bajeti hii imetengewa fedha na itaanza kujengwa katika bajeti tunayoanza. Hali kadhalika, barabara aliyoitaja ya Makete - Isyonje kwenda Mbeya pia imepangiwa bajeti na itatangazwa katika mwaka wa fedha ujao. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge barabara zote barabara zote mbili alizozitaja zipo na zimepangiwa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa mwaka ujao wa fedha, ahsante. (Makofi)

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA K.n.y. MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa barabara ya Njombe – Mdandu – Iyayi kuelekea Mbeya?

Supplementary Question 2

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Ni lini Serikali itakamilisha barabara ya Iringa bypass kwa kilometa 6.8 zilizobaki?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara uliyoitaja ya kilometa
6.9 ni barabara muhimu ambayo itatuondolea adha pale ambapo changamoto ikitokea kati ya Ruaha na Mjini pakikwama basi mji unakuwa umefunga. Na Mheshimiwa Mbunge anajua kwamba tayari tumeshaanza na katika bajeti tunayoanza, barabara hii utaendelea; lengo ikiwa ni kukamilisha hizo kilometa zilizobaki kwa ajili ya kuondoa hizo changamoto, ahsante.