Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 56 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 471 2021-06-22

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA K.n.y. MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa barabara ya Njombe – Mdandu – Iyayi kuelekea Mbeya?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Njombe (Ramadhani) – Mdandu – Iyayi yenye urefu wa kilometa 74 ilikamilika tangu mwaka 2015. Kwa sasa ujenzi unaendelea kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha ambapo jumla ya kilometa 14.11 kati ya kilometa 74 tayari zimejengwa kwa kiwango cha lami ikiwemo sehemu ya Mji wa kihistoria ya Mdandu.

Aidha, katika mwaka wa fedha 2020/2021 kipande cha kilometa 1.5 kinaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi milioni 929.288 na katika mwaka wa fedha 2021/2022 kipande kingine cha barabara chenye urefu wa kilometa 1.5 kinatarajiwa kuanza kujengwa na inakisiwa kugharimu shilingi milioni 929.288. Ahsante.