Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Kyetema – Katoro – Kyaka utaanza na kukamilika kwa kiwango cha lami kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Supplementary Question 1

MHE. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri, lakini majibu haya vilevile yaliwahi kutolewa huko nyuma kwa swali hilihili ambalo limewahi kuulizwa, lakini tukaambiwa hela imepatikana ya msanifu na msanifu huyo hakuonekana na barabara hiyo mpaka leo haijawahi kujengwa. Sasa naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, je, Wizara inafahamu umuhimu wa barabara au inajibu tu ilimradi kujibu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa vile Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka jana imeiweka barabara hii kwamba ijengwe kwa kiwango cha lami na kwa ville hata Ilani iliyopita ya mwaka 2015 ilikuwa na barabara hii, je, naweza leo kupata commitment ya Serikali kwamba ni lini ujenzi huu wa barabara hii kwa kiwango cha lami unaanza? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru, na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jasson Rweikiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi inatambua umuhimu wa barabara hii na ndio maana mwenyewe anafahamu kwamba ana vijiji karibu 29, vijiji 18 vipo katika barabara hii kwa hiyo ikijengwa ni wazi kwamba uhakika wa yeye kuendelea kuwa Mbunge wa Bukoba Vijijini utakuwa umetimizwa.

Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha 2020/2021 kuna fedha milioni 557 zilitengwa kwa ajili ya kuendelea kufanya maboresho ili barabara hii iendelee kupitika wakati wote.

Vilevile mwaka wa fedha 2021/2022 zimetengwa fedha zaidi ya milioni 217 kwa ajili ya kuendelea kufanya maboresho. Kwa hiyo, hii inaonesha kwamba Wizara inajua umuhimu wa barabara hii na ndio maana imekuwa ikitenga fedha kutoka mwaka hadi mwaka ili kuendelea kuiboresha ili wananchi wa Bukoba Vijijini waendelee kupata huduma hiyo ya barabara.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili; ametaka kujua commitment ya Wizara. Kwenye jibu la msingi nimesema barabara hii tayari kuna mhandisi mshauri ambaye atafanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Na barabara hii kuna wahandisi wawili ambao wamepatikana; Mhandisi consultant ambaye atafaya kazi ya kutoka Kyetema – Kanazi – Katoro – Kyaka yenye urefu wa kilometa 60.7 atafanya kazi hiyo ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Mheshimiwa Spika, mhandisi wa pili Age Consultant yeye atafanya kazi sehemu ya barabara ya Bukoba, Bosimbe na Maluku yenye urefu wa kilometa 19.

Kwa hiuyo, wahandisi hao wawili wakifanya kazi hii ikikamilika sasa tutaanza angalau kilometa chache kufanya kazi ya ujenzi wa lami katika eneo hili ili Mheshimiwa Mbunge Jasson Rweikiza aendelee kuwa na uhakika wa kuendelea kuwa Mbunge wa eneo hili, ahsante.