Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 56 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 470 2021-06-22

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Kyetema – Katoro – Kyaka utaanza na kukamilika kwa kiwango cha lami kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru na kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jasson Samson Rweikiza Mbunge wa Bukoba Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mhandisi Mshauri atakayefanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Kyaka 2 – Kanazi – Kyetema yenye urefu wa kilometa 60.7 amepatikana na anatarajiwa kusaini mkataba mwishoni mwa mwezi Juni, 2021. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya shilingi milioni 500 zimetengwa kwa ajili ya kuanza kazi hiyo. Baada ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamlika Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante.