Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itazalisha mbegu za mti wa mninga ili wananchi waweze kupanda na kuzalisha miti hiyo kibiashara?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Naipongeza Serikali kwa majibu mazuri sana ambayo wameyatoa hapa mbele ya Bunge, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza; miti hii inapatikana kwenye maeneo yaliyohifadhiwa na maeneo ambayo hayajahifadhiwa, yakiwemo mashamba ya watu binafsi na ardhi ambayo inamilikiwa na watu binafsi. Sasa swali langu; kwa nini Serikali isitoe ruhusa maalum itakayosimamiwa na Serikali za vijiji kwenye maeneo hayo ambayo hayajahifadhiwa ili watu waruhusiwe kuvuna miti wanayoimiliki kihalali kwa ajili ya matumizi ya ujenzi wa nyumba za asili pamoja na nyumba za kisasa bila kwanza kupata vibali vile vya maliasili kwa sababu maeneo hayo hayahusiani na maliasili? Kwa sababu matumizi yale siyo ya kibiashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili; kuhusu uvunaji wa miti kwenye maeneo yaliyohifadhiwa; kwa nini Serikali isitoe elimu kwanza kupitia mikutano ya hadhara na njia nyingine za mawasiliano ili wananchi wapate ufahamu wa kutosha wa namna ya kuomba vibali ili wasiingie migogoro mara kwa mara ya kuvunja sheria za nchi? Nashukuru sana.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, kwamba Serikali ipo kwa ngazi zote. Kuhusu swali lake linalosema kwa nini Serikali isitoe ruhusa kwenye maeneo yasiyohifadhiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo yote ambayo yana rasilimali za misitu yanahifadhiwa na Serikali ikiwemo Wizara ya Maliasili na Utalii, lakini kwenye ngazi za vijiji na maeneo ya wilaya, zinahifadhiwa na Serikali za Mitaa, zikiwemo halmashauri za wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye maeneo haya ambayo vibali vyake vinatolewa na Maliasili ni yale maeneo ambayo yanahifadhiwa na Wizara. Hata hivyo, kuna yale ambayo yanahifadhiwa na Serikali za Mitaa, vibali vyote huwa vinatolewa kwenye level ya vijiji na wilaya. Kwa hiyo wale wote ambao wanahitaji kupata vibali basi wawe wanakwenda kwenye maeneo hayo na pia watapata hivyo vibali.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwakumbushe tu kwamba maeneo yote yanahifadhiwa, siyo kwa ajili ya kutunzwa peke yake, lakini pia na uhifadhi wa mazingira pamoja na utunzaji wa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la pili, ameuliza kuhusu elimu; ni kweli kwamba Serikali imeendelea kutoa elimu mbalimbali kwa wananchi ili watambue umuhimu wa utunzaji wa miti. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mpango wa bajeti na fedha zilizoidhinishwa kipindi hiki tumeweka eneo la elimu ambalo tutapita kila maeneo ambayo yanazunguka hifadhi kuhakikisha kwamba wananchi wanapata elimu ya kutosha na namna ya kuomba hivi vibali vya ukataji miti. Ahsante.

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itazalisha mbegu za mti wa mninga ili wananchi waweze kupanda na kuzalisha miti hiyo kibiashara?

Supplementary Question 2

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Wananchi wangu wa Jimbo la Bunda Mjini, Alhamisi ya wiki iliyopita tembo wamekula mazao yao, hasa Kata za Bunda Stoo, Balili na Kunzugu. Wapo baadhi ambao wamefanyiwa tathmini ya mazao yao, je, ni lini Serikali itawalipa fidia yao?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Robert Maboto, Mbunge wa Bunda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshaanza kulipa malipo haya ya kifuta jasho na kifuta machozi na kulikuwa kuna malipo ya kipindi cha nyuma ambayo walikuwa wanadai na niliahidi hata kwa Mbunge mwenzie Mheshimiwa Esther Bulaya, kwamba nitafunga safari niende kwenye maeneo husika tukaangalie ni madai gani ambayo wanadai kisha Serikali iweze kuyalipa. Ahsante.