Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 55 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 464 2021-06-21

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itazalisha mbegu za mti wa mninga ili wananchi waweze kupanda na kuzalisha miti hiyo kibiashara?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umaarufu wa mti wa mninga katika matumizi ya shughuli za ujenzi na utengenezaji wa samani. Kutokana na umuhimu huo, Wizara kupitia TFS imeandaa mpango wa miaka mitano wa kuendeleza mti huo na miti mingine kibiashara kwa kuipanda kama ilivyo miti ya kigeni. Mpango huo unahusisha aina 56 za miti ya asili ikiwemo mninga ambapo kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 Wizara imetenga shilingi 60,000,000 kwa ajili ya kuzalisha mbegu za miti hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nia ya Wizara ni kuongeza kasi ya uzalishaji wa mbegu za miti ya asili ili wananchi waweze kuzipata kwa urahisi kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania zilizopo kwenye kanda mbalimbali hapa nchini. Aidha, Wizara itaendelea kuimarisha elimu ya upandaji wa mti wa mninga ili kuleta hamasa ya kupanda na kutunza miti hiyo. Serikali itahakikisha elimu ya utunzaji na uendelezaji wa miti ya mninga iliyopo katika maeneo ya mashamba ya wananchi inatolewa ili miti hiyo itunzwe kwa ajili ya kuzalisha mbegu ili kuwezesha wananchi kupanda miti ya mninga kibiashara.