Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mbulu – Haydom – Singida kwa lami, ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais tangu mwaka 2015?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, hiii ndiyo ile barabara ambayo nilitaka kuruka somersault humu ndani. Kwanza niishukuru Serikali kwa kutangaza hizi kilometa 25.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kwenye bajeti ya Serikali ziko kilometa 50;

Je, ni lini unatangaza tena slot iliyobaki ya kilometa 25?

Mheshimiwa Naibu Spika, na kwa kuwa amesema barabara hii ina kilometa 70,

Je, kilometa 20 zinazobaki point tano atatangaza lini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Flatei Grerory Massay Mbunge wa Mbulu Vijijini, kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru kwanza leo hajataka kuruka sarakasi. Na kama alivyoahidi Mheshimiwa Waziri wakati wa bajeti kwamba barabara hizi zitatangazwa ni kweli zimetangazwa, na hizo kilomita 25 zinaanza kujengwa kwa bajeti ya mwaka huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti ya mwaka tutakayoanza Julai pia kuna fedha imetengwa. Kwa hiyo tutaendelea na ujenzi kadri fedha itakapopatikana, lakini kwenye bajeti pia tumetenga. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kadri fedha itakapopatikana kilomita zote na barabara yote hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante sana.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mbulu – Haydom – Singida kwa lami, ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais tangu mwaka 2015?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Sibiti hadi Hydom kwa kiwango cha lami kwa sababu tayari ipo kwenye bajeti? Ahsante (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyouliza Mheshimiwa Flatei ndio mwendelezo wa barabara kutoka Hydom kwenda Daraja la Sibiti. Ni barabara ambayo inafanya kama kilomita 300 na kitu ambayo inaanzia Kolandoto, Lalago, Sibiti, Hydom, Mbulu hadi Karatu. Tayari tumeshaanza ujenzi, kwa maana ya daraja na kilomita zake takriban 25; na kwa hiyo kadri tutakavyoendelea kupata hela barabara hii tutaiunganisha yote kuwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.