Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 55 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 460 2021-06-21

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mbulu – Haydom – Singida kwa lami, ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais tangu mwaka 2015?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Mbulu - Hydom hadi Singida yenye urefu wa kilometa 160.5 inahudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS). Barabara hii imegawanyika katika sehemu kuu mbili za Mbulu – Haydom urefu wa kilometa 70.5 na Haydom – Singida urefu wa kilometa 90.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sehemu ya pili ya Mbulu –Haydom imetangazwa kwa ajili ya kumpata mkandarasi wa ujenzi kwa kuanza na kilometa 25 na sehemu zingine zilizobaki zitaendelea kuongezwa wakati sehemu ya kwanza ya kilometa 25 ikiendelea. Sehemu iliyobaki ya Haydom – Singida ipo katika hatua ya manunuzi ili kumpata mhandisi mshauri atakayefanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kabla ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante.