Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kuwa Wananchi wa Jimbo la Kiteto wananufaika na Miradi ya Maji safi na salama ili waweze kufikia azma ya asilimia 85 na asilimia 95 Vijijini na Mijini ifikapo Mwaka 2025?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru na ninashukuru sana kwa majibu mazuri sana ya Serikali; na nishukuru juzi tu wakati wa Mbio za Mwenge tulizindua miradi ya Wezamtima na kutembelea miradi mingine ya maji kule Nchinila. Pamoja na haya ninashukuru sana kwa majibu haya ambayo wananchi wangu wa Kibaya pale, na nniafurahi kusema watakuwa wamesikia majibu haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Je, ni lini sasa Serikali itajenga Bwawa la Dongo ambalo lipo kwenye mpango wa Mwaka huu wa Fedha 2021/2022. Lakini wakati huo huo pale pale Dongo tuna Mlima Njoge unatiririsha maji; na kwa kuwa tanki ambalo limejengwa ni zamani sana, ni la mwaka 1965, na katika Vijiji vya Dongo na Chang’ombe wananchi wameongeza; ni nini kauli ya Serikali kuhusu kujenga tanki kubwa la maji; pengine la lita laki moja, laki mbili ili wananchi hawa waendelee kunufaika wakati wanasubiria bwawa hili la Dongo ambalo tunasuburia kwa hamu sana? Ahsante sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Edward Olelekaita, Mbunge wa Kiteto kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipende kukushukuru kwa kukiri kazi kubwa ambayo imefanyika na hata Mwenge wetu wa uhuru umeweza kuzindua miradi ile. Lakini vilevile nipende kukujibu swali lako, kwamba ni lini bwawa la Dongo litafanyikwa kazi. Umeshajibu wewe mwenyewe kwamba mwaka ujao wa fedha tayari mpango mkakati umeuona uko pale hivyo tusubiri muda. Na kadri fedha itakavyokuja ndivyo kasi ya ujenzi wa lile bwawa itakuwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusiana na hili bwawa lililojengwa miaka ya 1965 tunafahamu ongezeko la wananchi ni kubwa. Tayari tuna mikakati ya kuja kukarabati tanki hilo, lakini vile vile kuongeza matanki mengine kadri fedha tutakavyopata, na mwaka ujao wa fedha naamini tutakuja kufanya hizi zote. Lengo ni kuona wananchi wanapata maji safi na salama ya kutosheleza na wananchi wote wapate maji bombani.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kuwa Wananchi wa Jimbo la Kiteto wananufaika na Miradi ya Maji safi na salama ili waweze kufikia azma ya asilimia 85 na asilimia 95 Vijijini na Mijini ifikapo Mwaka 2025?

Supplementary Question 2

MHE: ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili na mimi nipate kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naishukuru Serikali kwa kutupatia fedha kwa ajili ya maji ya Mji wa Liwale. Hata hivyo mpaka leo DDCA wametutia changa la macho, ni mwezi wa sita huu hawajaja; na Mheshimiwa Waziri ameniambia kwamba kuna uwezekano tukachukua watu binafsi wakaanza kuchimba pale. Lakini nimewasiliana na Mhandisi anasema asilimia 30 ya fedha hizo tayari DDCA walishachukua na walishaingia mitini.

Je, ni lini DDCA watakuja kutuchimbia maji Wilaya ya Liwale?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Zuberi ni jana tu tumeongea na Mheshimiwa Waziri amekupa hayo maelekezo. Kwa hiyo nipende tu kuongezea pale alipoongea bosi wangu kama alivyokuhakikishia, pale DDCA wanapozidiwa kazi basi watu binafsi tutawapa vibali ili waweze kuja kuchimba hivi visima. Na visima hivi mwaka ujao wa fedha ninaamini vitachimbwa na mambo yatakaa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na fedha iliyochukuliwa na DDCA fedha ikichukuliwa maana yake ni lazima kazi ije ifanyike. Kwa hiyo kwa ile asilimia ambayo wamechukua lazima watakuja kufanya hiyo kazi.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kuwa Wananchi wa Jimbo la Kiteto wananufaika na Miradi ya Maji safi na salama ili waweze kufikia azma ya asilimia 85 na asilimia 95 Vijijini na Mijini ifikapo Mwaka 2025?

Supplementary Question 3

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi naomba kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mji Mdogo wa Matui Wilaya ya Kiteto una wakazi wengi na unaendelea kukua kwa kasi.

Nini kauli ya Serikali juu ya upatikanaji wa uhakika wa maji safi na salama kwa wananchi wa Matui pamoja na viunga vyake?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Mbunge wa Viti Maalum vijana kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo haya ya Matui huko Kiteto nayyo ni miongoni mwa maeneo ambayo Wizara imetoa jicho la kipekee kabisa. Tunafahamu kuwa ni maeneo ambayo watu wameongezeka sana, hivyo mwaka ujao wa fedha kila eneo tutalitupia jicho, na kwa eneo hili la Matui pia tutalipa kipaumbele.