Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 54 Water and Irrigation Wizara ya Maji 452 2021-06-18

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: -

Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kuwa Wananchi wa Jimbo la Kiteto wananufaika na Miradi ya Maji safi na salama ili waweze kufikia azma ya asilimia 85 na asilimia 95 Vijijini na Mijini ifikapo Mwaka 2025?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edward Kisau Olelekaita Mbunge wa Kiteto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Manyara ni miongoni mwa maeneo kame nchini ambayo chanzo kikuu cha maji ni maji chini ya ardhi. Huduma ya maji ya uhakika katika Wilaya Kiteto kwa upande wa vijijini inapatikana vijiji 35 kati ya 63, sawa na asilimia 53 kwa mjini ni asilimia 44.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa vijijini, Serikali imepanga kutekeleza miradi mitano au zaidi kila mwaka ili huduma ya maji ifike katika vijiji vyote 63 na kufikia lengo la asilimia 85 au zaidi. Kwa upande wa Mji wa Kibaya kwa mwaka 2021/2022, Serikali imepanga kutekeleza mradi ambao utahusisha ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji ambapo huduma ya maji itakayopatikana itakidhi mahitaji ya wananchi wa Kibaya kwa asilimia 95 au zaidi ifikapo mwaka 2025.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuboresha huduma ya maji katika maeneo kame, Serikali itatekeleza mpango wa ujenzi wa mabwawa madogo na makubwa na ukubwa wa kati kwa ajili ya kuvuna maji ya mvua na kuongeza uhakika wa upatikanaji wa maji wakati wote.