Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Tarime hadi Serengeti kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali madogo tu ya nyongeza: -

(a) Serikali imetangaza tarehe 4 Juni zabuni je, ni lini sasa kilometa 76 zilizobaki zitafanyiwa kazi? (Makofi)

(b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha barabara hii inaendelea kupitika wakati wote. Ahsante. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Zephania Ghati Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Rais kwamba ametoa kibali barabara hii imetangazwa inajengwa kwa awamu, kwa kuanzia na kilometa 25 tuna bilioni Sita za kulipa advance payment baada ya kumpata mkandarasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia swali lake la pili kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Mkoa wa Mara kupitia TANROADS imetenga shilingi milioni 411 kwa ajili ya kuendelea kufanyia maboresho barabara hii hadi hapo itakapokuwa imekamilika. Ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Tarime hadi Serengeti kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa, sera ya Serikali ni kuunganisha kwa kiwango cha lami barabara za Mikoa na Wilaya na kwa kuwa barabara ya Idete – Iringa ni barabara ambayo inaunganisha Majimbo matatu, Iringa Mjini, Jimbo la Kalenga na Jimbo la Kilolo.

Je, ni lini sasa Serikali itaijenga kwa kiwango cha lami barabara hii kwa sababu kwanza ni ya kiuchumi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA
M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum maarufu wa Mkoa wa Iringa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba barabara aliyoitaja ni muhimu sana, na mpango wa Serikali ni kuunganisha mkoa na mkoa na wilaya na wilaya.

Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwa niaba ya Serikali, kwamba fedha zikipatikana wakati wowote barabara hizi zote muhimu zitajengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante sana.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Tarime hadi Serengeti kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itaikumbuka Barabara ya Bujera – Masukulu mpaka Matwebe katika Wilaya ya Rungwe kuweza kutujengea? Mheshimiwa Waziri naomba jibu la Serikali.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Mkoa wa Mbeya, wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Rungwe mimi nimefika, na maeneo ya Mbeya kwa ujumla wake; na tumekubaliana kwamba tunapotaka kujenga barabara za eneo hili usanifu wa kina lazima ufanyike kwa sababu ya miundombinu yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mbheshimiwa Sophia kwamba, pesa ikipatikana wakati wowote, barabara hii itajengwa kiwango uliyoitaja muhimu sana kwa watu wa Rungwe cha lami. Ahsante.