Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 52 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 436 2021-06-16

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Tarime hadi Serengeti kwa kiwango cha lami?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Tarime – Mugumu (Serengeti) ina jumla ya urefu wa kilometa 87.14 ambapo sehemu ya barabara hiyo yenye urefu wa kilometa
10.7 tayari imejengwa kwa kiwango cha lami na kilometa 76.44 zilizobaki zimejengwa kwa kiwango cha changarawe. Aidha, Serikali imekamilisha ujenzi wa daraja la Mara lililopo katika barabara hii lenye urefu wa meta 94 na barabara za maingiliano za daraja hilo zenye urefu wa kilometa 1.8.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zabuni kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kilometa 25 nje ya kilometa 76.44 zisizokuwa na lami za barabara hiyo imetangazwa tarehe 4 Juni 2021. Taratibu za manunuzi zikikamilika kazi za ujenzi zitaanza mara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali itaendelea na ujenzi wa barabara hii kwa sehemu itakayobaki kadri ya upatikanaji wa fedha utakavyopatikana.