Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:- Je, uwepo wa Kiwanda cha kuua mazalia ya Mbu (Tanzania Biotech Product Limited) umesaidia vipi mapambano dhidi ya Malaria nchini?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Kwa kuwa, azma nzima ya kuondoa malaria siyo kupunguza bali ni kumaliza kabisa na Zanzibar wamefanikiwa. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kugawa viuadudu hivyo wakati wa weekend zote za kufanya usafi majumbani kwa watu? (Makofi)

Swali la pili, kwa kuwa Kamati ya Bunge ilipotembelea kwenye kiwanda hicho ilikuta bado Halmashauri nyingi hazijalipa mikopo ambayo walichukua. Ni lini sasa Serikali italipa ili kiwanda kile kiweze kuendelea vizuri. (Makofi)

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE
NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunaelekea kwenye elimination na ndiyo mkakati wa Serikali na tumejipanga pamoja na wadau wetu kwamba tunapata fedha kwa ajili ya kufanya haya masuala ya kununua hivi viuadudu endelevu kwa ajili ya kuelekea kwenye elimination. Kwa mfano, Serikali ya Uswiss kwenye mpango wake wa Miaka Nne, 2021- 2024 kuna bilioni 4.4 zimetengwa ambapo bilioni 3.7 zitatumika kununua lita 284,810 kwa ajili ya utekelezaji huo. Sasa hivi tunaandika andiko ambalo litagharimu bilioni 294 kwenye Mwaka wa Fedha ujao tutalileta kwa wastani wa bilioni 59 kila mwaka tuweze kuwa na utaratibu wa kuwa tunapuliza haya mazalia mpaka kila kitu kiishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu haya masuala ya Halmashauri kutokulipa kama nilivyosema kwenye jibu la msingi zimetengwa bilioni 2.7 tutasimamia walipe yale madeni lakini waendelee kuchukua na kupewa viuadudu vingine vya ziada. Ahsante.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:- Je, uwepo wa Kiwanda cha kuua mazalia ya Mbu (Tanzania Biotech Product Limited) umesaidia vipi mapambano dhidi ya Malaria nchini?

Supplementary Question 2

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa Mikoa ambayo inaongoza kwa maambukizi ya malaria ni pamoja na Mkoa wa Mtwara. Nataka kujua mkakati wa Serikali kuhakikisha Mkoa ule unaondoka katika janga hilo la ugonjwa wa malaria. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE
NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mkoa wa Mtwara ni kati ya Mikoa ambayo ina maambukizi makubwa ya malaria, tunalitambua hilo, iko Mikoa ya Lindi, Katavi na mingine mingi. Tunaipa kipaumbele kwa hizi rasilimali tulizonazo hatutazitumia tu hivi randomly. Kwa mfano Arusha, Manyara, pamoja na Moshi wenyewe wameshakwenda kwenye elimination. Kwa hiyo tutaongeza nguvu sana ku- adress haya masuala ya Mikoa ambayo bado maambukizi yapo juu. Tutashirikiana pia na Wizara ya Mazingira kwa sababu suala hili ni mtambuka kuhakikisha kwamba tunaifikia hii Mikoa tushushe kama Manyara, Arusha na Moshi. Ahsante. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri, kaa hapo hapo. Sasa hivi kuna mtindo watu wanapita majumbani wanamwaga dawa kwa barua za Halmashauri asilimia kubwa ya dawa hizo ni maji. Hilo nalo mlidhibiti.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE
NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nimepokea na nawatumia salamu huko walipo. Tunaanza kuwafuatilia leo hii tujue walitumwa na nani na kiwango cha ubora wa hizo dawa wanazomwaga. Nasema waache maana Serikali iko kazini. Ahsante.