Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMUS H. MAGANGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza barabara zote mbovu zilizopo katika Jimbo la Mbogwe?

Supplementary Question 1

MHE. NICODEMUS H. MAGANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, nakushkuru Mheshimiwa Waziri, uzuri umejibu halafu umefanya ziara kwangu, hizo barabara zote ulizozisema ni mbovu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza ambayo ni hatarishi sana, daraja la Budoda halipitiki toka kwenye kampeni. Je, Serikali haina mfuko wa dharura kwenda kurekebisha madaraja ambayo yanawafanya wananchi kupoteza Maisha? Kuna Kata ya Ngemo, Mtonya pamoja na Ludembela, kuna madaraja mpaka sasa hivi hayapitiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa wewe Mheshimiwa Naibu Waziri, ulifika kwenye jimbo langu na ukajionea na tulizama mara tatu. Je, kwa sasa hivi na bunge linakwenda kuisha, nikawaambieje wananchi kulingana na ubovu wa barabara hizi ambazo hazipitiki?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nicodemus Maganga, Mbunge wa Mbogwe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ameuliza kwamba daraja la Budoda halipitiki kwa muda mrefu tangu kipindi cha kampeni, kwa hiyo akauliza kama hakuna fedha za dharura. Niseme tu Mheshimiwa mbunge nimelipokea jambo lako na ninalikabidhi kwa TARURA Makao Makuu, ili waende wakafanya tathmini hiyo na watuletee taarifa ili tutafute fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la Pili ameuliza atawaambi nini wananchi, kwa kuwa bunge linakwisha na barabara zake bado hazipittiki. Nenda kawaeleze tu kwamba Serikali tumejipanga kuhakikisha kwamba tunamaliza matatizo ya barabara maeneo mengi nchini. Na katika hatua ya awali ambayo tulioichukuwa ni kupeleka fedha milioni 500 kwenye kila Jimbo, ambazo zitakwenda kujenga barabara za lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili waeleze wananchi wako kwamba, mara baada ya bajeti ya Serikali kupita, kikiwemo kile kifungu maalum cha kuongezea fedha za TARURA, tutaongeza fedha katika Jimbo lako ambazo zitasaidi zaidi zile barabara ambazo ni mbovu. Ahsante sana.