Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Je, ni lini Kata 16 zisizo na mawasiliano ya simu katika Wilaya ya Urambo zitapatiwa mawasiliano ya simu na kuwaondolea wananchi adha ya kutokuwa na mawasiliano kwa muda mrefu? Je, ni kwa nini kuna maeneo yenye minara ya mawasiliano ya simu lakini kuna matatizo ya mawasiliano?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake lakini bado ningeomba kwa kuwa maisha ya sasa yanategemea sana matumizi ya simu na wahusika wanaathirika kwa kiasi kikubwa naomba niyataje maeneo hasa ambayo yanahitaji kuchukuliwa hatua haraka iwezekanavyo, Kata ya Itundu, hasa Katuli, Ilani, Kiloleni, Mwinyi, Kalembela, Jumbe na Kikwete Kata ya Muungano ni Muungano yenyewe, Magulungu, Isenda, Utenge na Kangeme, Kata ya Usisya ni Usisya Kati, Mabundulu, Katungulu na Majengo. Kata ya Uyogo ni Uyogo yenyewe, Igembesabo, Kasela, Igunguli na Mirambo, Kata ya Ugala ni Ugala yenyewe Izengamatogile na Isogwa, Songambele, Mlangale na Ukwanga na Kata ya Kapilula ni Kata yote, naomba lini wanapatiwa mawasiliano watu wa Urambo. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya kwa ajili ya wananchi wa Urambo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli alichokiongea Mheshimiwa Mbunge ni kweli kabisa, kwasababu tayari tarehe 16 Machi 2021 nilifanya ziara katika Jimbo lake la Urambo, na kweli nikagundua kuna maeneo ambayo bado yana changamoto ya mawasiliano. Lakini katika maeneo ambayo tuligundua yana changamoto ya mawasiliano, tulitoa maelekezo ili tathmini ifanyike na kuhakikisha kwamba wananchi wa Urambo hawapitwi mbali na huduma ya mawasiliano kwa ajili ya kujiletea maendeleo kupitia mtandao wa mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Je, ni lini Kata 16 zisizo na mawasiliano ya simu katika Wilaya ya Urambo zitapatiwa mawasiliano ya simu na kuwaondolea wananchi adha ya kutokuwa na mawasiliano kwa muda mrefu? Je, ni kwa nini kuna maeneo yenye minara ya mawasiliano ya simu lakini kuna matatizo ya mawasiliano?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Jimbo la Tabora Mjini lina kata 29 na
vijiji 41, na katika vijiji hivyo vingi havina mawasiliano ya simu na vijiji vingine vipo karibu kabisa, kilomita mbili tu kutoka mjini lakini bado ni vigumu kupata mawasiliano; mathalani kata ya Itetemya. Ninaomba kuuliza;

Je, ni lini Serikali itatufanyia mpango wa kuongeza angalau minara ili mawasiliano yaweze kuwa mazuri? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA
HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakasaka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya mawasiliano ni takriban nchi nzima ina changamoto mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna changamoto ambazo zinatokana na teknolojia iliyowekwa katika eneo husika, lakini pia mnara uliowekwa pale inategemea kwamba uliwekwa katika wakati upi, kwamba iawezekana kulikuwa na population ya watu wachache na sasa wameongezeka sasa mnara unaweza ukazidiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunafahamu kabisa kwamba kuna maeneo ambayo kutokana na sababu za kijiografia unakuta kwamba katika kata moja mawasiliano yapo katika vijiji sita lakini Kijiji kimoja kinakuwa kinakosa mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Serikali kupitia Wizara yetu imeanza kufanya utafiti wa kujiridhisha ili tuweze kupata teknolojia ambayo tutakuwa tunafikisha huduma ya mawasiliano katika zile sports ambapo unakuta kwamba ni Kijiji kimoja tu ambacho kimekosa mawasiliano lakini tufikishe kwa teknolojia ambayo ni nafuu na yenye gharama nafuu. Waheshimiwa Wabunge pia tuweze kusaidiana kuhakikisha kwamba tunawaelewesha wananchi wetu kujua kwamba mawasiliano yatafika kwasababu bahati nzuri mmetusaidia kupitisha bajeti ambayo itatufikishia mawasiliano katika vijiji vyetu.