Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 51 Works, Transport and Communication Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 426 2021-06-15

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:-

Je, ni lini Kata 16 zisizo na mawasiliano ya simu katika Wilaya ya Urambo zitapatiwa mawasiliano ya simu na kuwaondolea wananchi adha ya kutokuwa na mawasiliano kwa muda mrefu?

Je, ni kwa nini kuna maeneo yenye minara ya mawasiliano ya simu lakini kuna matatizo ya mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Urambo lina jumla ya Kata 18 ambapo Kata zote zina huduma ya mawasiliano isipokuwa vijiji baadhi katika Kata Tisa za Kiloleni, Itundu, Imalamakoye, Ugalla, Vumilia, Nsondo na Uyogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata za Utundu na Ukondamoyo zitafikishiwa huduma za mawasiliano na kampuni ya simu ya Vodacom ifikapo Oktoba, 2021, Kata za Nsondo na Uyogo zitafikishiwa huduma za mawasiliano na kampuni ya Airtel ifikapo Oktoba, 2021, Kata ya Vumilia itafikishiwa huduma za mawasiliano kupitia kampuni ya simu ya Halotel ifikapo Septemba, 2021 pamoja na Kata ya Ugala itakayofikishiwa huduma na kampuni ya simu ya TTCL ifikapo Septemba, 2021. Aidha Kata za Kiloleni na Imalamakoye zitaingizwa kwenye miradi ya mfuko itakayotekelezwa kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sababu mbalimbali zinazoweza kusababisha kukosekana huduma ya mawasiliano kwenye maeneo yenye minara ya simu ikiwa ni pamoja na hali ya kijiografia ya eneo husika kama vile uwepo wa milima, mabonde na uoto wa asili wenye miti mirefu ambayo huzuia huduma za mawasiliano. Hali ya kukosekana kwa nishati ya umeme wa uhakika pia inaweza kusababisha minara kushindwa kutoa huduma za mawasiliano. Ahsante.