Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Jimbo la Tunduru Kusini lina Vijiji sita kati ya 65 vyenye umeme. (a) Je, ni lini REA Awamu ya Tatu utaanza? (b) Je, ni lini umeme wa ujazilizi wa maeneo ambayo bado umeme haujafika hasa Vitongoji vya Vijiji vya Azimio, Chiwana, Umoja, Mkandu, Mbesa, Airport, Namasalau, Tuwemacho, Ligoma, Mchuruka na Makoteni vitapatiwa umeme?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nishukuru Serikali kwa kupeleka mkandarasi amesharipoti tarehe 11 Mwezi huu. Kwa kuwa Serikali inaenda kutekeleza mradi huu katika vijiji vyote vya Jimbo la Tunduru Kusini na Tunduru kwa ujumla na tatizo la Umeme Tunduru kukatika katika ni jambo la kawaida.

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga substation pale Tunduru Mjini ili kutoa huduma hii kwa vijiji vyote kwa sawasawa? (Makofi)

Swali la pili, kwa kuwa REA imeanza kutekelezwa katika vijiji vyote vilivyopo Jimbo la Tunduru Kusini pamoja na vijiji vya Azimio, Semeni, Angalia Je, Serikali sasa haioni kuna haja sasa ya kuweza kutoa tamko la kuweza kuisaidia TANESCO kwa asilimia 100 ili waweze kutoka huduma hiyo kwa shilingi 27,000?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Daimu Mpakate Mbunge wa Tunduru kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza kuhusu hoja ya kupeleka substation tuichukue tukaifanyie mkakati na upembuzi yakinifu na kuona kama ujenzi wa substation peke yake ndio utasaidia kutokatika kwa umeme katika maeneo hayo au njia nyingine inaweza ikaboresha kwa sababu pengine kama umeme unaofika ni mkubwa wa kutosha maana yake tunatakiwa kuboresha miundombinu badala ya kujenga substation. Tunalichukua tutaenda kulifanyia kazi na tutaweza kufikisha huduma nzuri kabisa kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la pili tayari Serikali imeshatoa maagizo na maelekezo ya kuunganisha umeme kwa wateja wote kwa shilingi 27,000, katika bajeti iliyowasilishwa na Wizara ya Nishati kwa niaba ya Serikali ilisemwa hapa wazi na Mheshimiwa Waziri kwamba maeneo yote itakuwa ni shilingi 27,000 isipokuwa Dar es Salaam City Centre. Tayari wenzetu wa TANESCO wametoa circular kwa Meneja wa Wilaya na wa Mikoa kuhakikisha kwamba agizo hilo linatekelezwa na tunafahamu linaendelea kutekelezwa, lakini pale Waheshimiwa Wabunge ambapo bado mnaona changamoto basi tuwasiliane ili tuweze kuchukua hatua kwa sababu mambo mengine yanahitaji kusimamiwa kwa ajili ya manufaa ya wananchi. (Makofi)

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Jimbo la Tunduru Kusini lina Vijiji sita kati ya 65 vyenye umeme. (a) Je, ni lini REA Awamu ya Tatu utaanza? (b) Je, ni lini umeme wa ujazilizi wa maeneo ambayo bado umeme haujafika hasa Vitongoji vya Vijiji vya Azimio, Chiwana, Umoja, Mkandu, Mbesa, Airport, Namasalau, Tuwemacho, Ligoma, Mchuruka na Makoteni vitapatiwa umeme?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii niweze kuuliza swali la nyongeza. Mkoa wa Simiyu una vijiji 470 na vijiji vilivyopata umeme ni 332 vimeshapata umeme vijiji vilivyobaki ni 138.

Je, ni lini Serikali itakamilisha kupeleka umeme katika vijiji vilivyobaki. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Simiyu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tulivyosema ni kweli kwamba kuna maeneo bado hayajapata umeme katika vijiji takribani kama 1,500 nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba hivyo vijiji 132 ambavyo bado havijapata umeme kwa Mkoa wa Simiyu na vyenyewe vitapelekewa umeme kabla ya mwezi Desemba 2022 kwa sababu tayari mkandarasi tumempata na tunaamini amesharipoti site yupo katika hatua za kwanza za kufanya survey kuhakiki kwamba vijiji vimechukuliwa na baada ya hapo kazi itafanyika kwa muda uliopangwa na kukamilisha umeme kufikia Desemba 2022. (Makofi)