Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 51 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 425 2021-06-15

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: -

Jimbo la Tunduru Kusini lina Vijiji sita kati ya 65 vyenye umeme.

(a) Je, ni lini REA Awamu ya Tatu utaanza?

(b) Je, ni lini umeme wa ujazilizi wa maeneo ambayo bado umeme haujafika hasa Vitongoji vya Vijiji vya Azimio, Chiwana, Umoja, Mkandu, Mbesa, Airport, Namasalau, Tuwemacho, Ligoma, Mchuruka na Makoteni vitapatiwa umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini lenye sehemu (a) na
(b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa mradi wa kupeleka umeme wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa Pili ulianza mwezi Machi, 2021. Mradi huu utakamilika ifikapo mwezi Desemba, 2022. Katika jimbo la Tunduru Kusini Vijiji vyote vilivyobaki vitapelekewa umeme kupitia mradi huu wa REA-III unaoendelea kupitia Kampuni Mbili za Wakandarasi M/S JV Guangdong Jianneng Electric Power Engineering CO. LTD na White City International Contractors LTD. Gharama ya Mradi ni shilingi bilioni 27.25.

Mheshimiwa Mwenyekiti, usambazaji wa umeme wa ujazilizi katika vijiji vya Jimbo la Tunduru Kusini vikiwemo vitongoji vya Vijiji vya Azimio, Chimwana, Umoja Mkandu, Mbesa, Airport, Namesalau, Tuwemacho, Ligoma, Mchuruka na Makoteni utaanza mwezi Septemba, 2021 na kukamilika mwezi Desemba, 2022.