Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza Sera ya Afya ya kuwa na Kituo cha Afya kwa kila Kata ili kupunguza vifo vya Mama na Mtoto?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwa kuwa Naibu Waziri amejibu hapa kwamba, ni Sera ya Serikali kwamba kuwe na zahanati kwa kila kijiji, lakini pia, kituo cha afya kwa kila kata. Wilaya ya Kyerwa yenye kata 24 ina zahanati tatu, yenye vijiji 99 ina zahanati 23. Ningependa kujua je, kwa wilaya ya Kyerwa hiyo sera inatekelezwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni mkakati gani Serikali ilionao kuhakikisha wananchi wa Kyerwa nao wananufaika na Sera ya Serikali ya kuwa na huduma ya afya kila kijiji, kila kata? Nakushukuru.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge. Kama ambavyo nimejibu katika maswali ya msingi kwamba, Serikali katika kipindi cha miaka mitano imejenga zahanati zaidi ya 1,200 vituo vya afya zaidi ya 488 na hospitali za halmashauri zairi ya 102, lakini mkakati huu unaendelea kutekelezwa na Halmashauri hii ya Kyerwa ni miongoni mwa halmashauri ambazo zitapewa kipaumbele kuhakikisha vijiji vyake na kata zinapata vituo vya afya ili kusogeza huduma za afya kwa wananchi. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, awamu zinazofuata tutaendelea kuongeza kasi, lakini pia kuipa kipaumbele halmashauri ya Kyerwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili. Mkakati wa Serikali ni huo wa kuhakikisha kwamba, sasa kila kijiji, lakini pia kila kata na kila halmashauri inapata vituo vya huduma za afya, ili kusogeza huduma kwa wananchi. Nakushukuru.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza Sera ya Afya ya kuwa na Kituo cha Afya kwa kila Kata ili kupunguza vifo vya Mama na Mtoto?

Supplementary Question 2

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa nafasi na niipongeze Serikali kwa juhudi madhubuti za kuboresha ujenzi wa vituo vya afya, zahanati pamoja na hospitali:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Misenyi ni wilaya ambayo ina kata 20, lakini mpaka sasa inavyo vituo vya afya viwili. Sasa ni lini zamu ya Wilaya ya Misenyi itafikiwa angalao kuongezewa vituo vya afya kwa juhudi kubwa ambazo zimekuwa zikifanywa na Serikali?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Florent Kyombo, Mbunge wa Nkenge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo hili la Nkenge na Halmashauri ya Misenyi kwa ujumla wake Serikali imeweka kipaumbele cha kuhakikisha inafanya tathmini ya maeneo ambayo yatapewa kipaumbele cha kuanza kujenga zahanati, lakini pia vituo vya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali katika mwaka ujao wa fedha imetenga kujenga vituo vya afya 121, lakini katika miaka mingine inayofuata ya fedha pia, tutahakikisha tumeweka kipaumbele cha kujenga vituo vya afya kwa hivyo, Jimbo hili la Nkenge na Halmashauri ya Misenyi pia, ni moja ya halmashauri ambazo zitapewa kipaumbele. Nashukuru.