Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 51 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 422 2021-06-15

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza Sera ya Afya ya kuwa na Kituo cha Afya kwa kila Kata ili kupunguza vifo vya Mama na Mtoto?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutekeleza Sera ya Afya ya kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji na Kituo cha Afya kwa kila Kata kwa awamu ambapo kuanzia mwaka wa fedha 2015/2016 hadi 2020/2021 Serikali imejenga Zahanati 1,281, Vituo vya Afya 488 na Hospitali za Halmashauri 102. Mpango huu umewezesha kuongeza Vituo vya Afya katika Mamlaka za Serikali za Mitaa vyenye uwezo wa kutoa huduma za dharula za upasuaji kutoka Vituo 115 Disemba 2015 hadi Vituo 352 Juni 2021 na hivyo kuchangia katika kupunguza vifo vya mama wajawazito na Watoto. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali itaendelea na ujenzi wa vituo vya afya 121 na kiasi cha shilingi billioni 27.75 kimetengwa kwa ajili ya umaliziaji wa maboma 768 ya zahanati kote nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali ni kuendelea kutenga fedha za ujenzi wa vituo vya afya kwa awamu. Nakushukuru.