Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI K.n.y. MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza ahadi iliyotolewa na Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa Barabara ya Bomang’ombe – Rudugai – Chekimaji – Kikafu chini – Kawaya – Mijengweni – Shing’oro Mferejini hadi Makoa?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nina maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya Ndugu yetu pia:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza nauliza kwa kuwa, tayari barabara ya Mferejini – Narumu – Takri – Lyamungo hadi Makoa imeshatengewa shilingi milioni 500 kwa ujenzi wa kiwango cha lami. Je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa hivi kuongeza pesa mwaka huu wa fedha, ili hiyo barabara ikamilike kwa kiwango cha lami?

Mheshimiwa Mwenyekiti, na swali la pili, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa International School kwa Raphaeli, Umbwe, inayounganisha na hii Barabara ya Mheshimiwa Mafuwe kule Lyamungo kwa kiwango cha lami? Ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa hii barabara inayoishia pale Mto Sere?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Profesa Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ameeleza, kwanza ametambua kwamba, Serikali tumepeleka fedha milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya lami. Na kikubwa ambacho ameomba tu ni kwamba, je, Serikali ni namna gani tutaongeza fedha kwa ajili ya barabara hiyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, moja, tuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mama yetu Samia Hassan Suluhu kwa kutoa fedha milioni 500 kwa majimbo yote nchini kwa ajili ya barabara kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili kwenye jambo hili tuombe Bunge lako tukufu mpitishe bajeti kuu, ili yale mapendekezo yaliyoletwa na Wizara ya Fedha ya kuongezea TARURA fedha katika kile chanzo cha shilingi 100 iweze kupita maana tutapata fedha. Na hizi fedha tutakazopata maana yake tutakwenda kuongeza barabara katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo hili ejeo ambalo mmeliainisha hapo. Kwa hiyo, ombi letu kwenu mpitishe bajeti kuu na sisi tutafanyia kazi maombi yote ambayo Waheshimiwa Wabunge mmeyaleta kwetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili ameeleza hii Barabara ia International School kupitia Umbwe na hayo maeneo ambayo ameyaainisha ambayo yako katika jimbo lake:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge hivi ninavyozungumza kazi nzuri ambayo ulikuja Ofisini kwetu na ukatuomba tumeanza kwanza kujenga mifereji katika barabara hiyo na itakavyokamilika maana yake tutaipandisha hadhi kwa kuiongezea viwango vile ambavyo vinastahili. Kwa hiyo, ndio kazi ambayo tumedhamiria kuifanya na tutaifanya kwa wakati wote, ahsante sana.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI K.n.y. MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza ahadi iliyotolewa na Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa Barabara ya Bomang’ombe – Rudugai – Chekimaji – Kikafu chini – Kawaya – Mijengweni – Shing’oro Mferejini hadi Makoa?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na ninakubaliana na aliyosema Naibu Waziri:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa barabara hizi ziko kwenye tambarare ya Kilimanjaro na mvua zote zinazonyesha mlimani zinashuka chini na kufagia changarawe yote iliyowekwa na TARURA. Na kwa kuwa, Barabara ya kutoka Hai kwenda Rundugai inaunganisha Barabara ya TPC ambayo ni ya lami.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kabisa kuanza barabara hiyo kwa lami kuliko kila wakati kumalizia hela za Serikali kwenye changarawe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Kilimanjaro, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ameeleza concern njema kabisa yenye nia njema. Niseme kwamba, tumelipokea ombi lako tutakwenda kufanya tathmini, ili tuingize katika mipango inayofuatia ya kuhakikisha tunaiondoa hiyo adha. Sio kila wakati tu hizi barabara zetu zikawa zinaondolewa na mvua kutokana na ile changamoto ya udongo au kifusi kwa hiyo, tunachokitaka sisi ni kuhakikisha kwamba, hizi barabara zinatengenezwa katika kiwango ambacho muda wote zitakuwa zinapitika.

Kwa hiyo, nilipokee hilo na tutaliingiza katika mpango, ahsante.