Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 51 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 420 2021-04-15

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI K.n.y. MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza ahadi iliyotolewa na Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa Barabara ya Bomang’ombe – Rudugai – Chekimaji – Kikafu chini – Kawaya – Mijengweni – Shing’oro Mferejini hadi Makoa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Bomang’ombe – Rudugai – Chekimaji – Kikafu Chini – Kawaya – Mijengweni hadi Shing’oro Mferejini hadi Makao zimesajiliwa kwa majina ya Bomang’ombe – Kikafu Chini na ina urefu wa kilomita 26.53.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Shing’oro – Mijengweni hadi Makoa yenye urefu wa kilomita 12.7 na Barabara ya Mferejini – Makoa yenye urefu wa kilomita 21 ni barabara muhimu katika Halmashauri ya Hai na zinahudumiwa na Wakala wa Barabara Vijijini wa Wilaya ya Hai. Serikali inatambua kuwa barabara hizi ni miongoni mwa barabara zilizoahidiwa kujengwa kwa kiwango cha lami katika ahadi za Rais na Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kutekeleza ahadi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuzifanyia matengenezo barabara hizo ili kuhakikisha zinapitika katika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2020/2021, TARURA Halmashauri ya Hai iliidhinishiwa shilingi milioni 72 kwa ajili ya matengenezo ya Barabara ya Bomang’ombe – Kikafu Chini kipande chenye urefu wa kilomita 14 kwa shilingi milioni 35 kwa ajili ya matengenezo ya Barabara ya Shing’oro – Mijengweni kipande chenye urefu wa kilomita 4 na sShilingi milioni 67.5 kwa ajili ya matengenezo ya Barabara ya Mferejini – Makoa kipande chenye urefu wa kilomita 6.4 ambapo matengenezo ya barabara hizo yanaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022, TARURA Halmashauri ya Hai imetengewa jumla ya shilingi milioni 628.2 kwa ajili ya matengenezo ya Barabara ya Bomang’ombe – Kikafu Chini kipande chenye urefu wa kilomita 10 na boksi kalvati moja la Shing’oro – Mijengweni kipande chenye urefu wa kilomita 8 na ujenzi wa barabara ya Mferejini – Makoa kwa kiwango cha changarawe kwa kilomita 10.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi na kutekeleza ahadi za Rais za ujenzi wa barabara za lami katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Halmashauri ya Hai.