Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza: - Sekta ya Afya nchini ina upungufu wa Watumishi wapatao 16,000:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na changamoto hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. MWAMTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa moja ya changamoto ambazo zinasababisha kukosekana kwa watumishi kwenye sekta yetu ya afya ni pamoja na vifo, kustaafu na ujenzi wa vituo vya afya pamoja na zahanati. Na kwa kwakuwa bado tunaendelea na ujenzi wa vituo vya afya, je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kasi ya ujenzi wa vituo vya afya inaendana na kasi ya kuajiri watumishi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau mwaka 2017/2020 wameajiri watumishi 12,868 na wadau hao ni kama Benjamin Mkapa, AMREF na MDH. Je, ni upi mchango wa wadau hao katika ajira kwa sekta hii ya afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA(MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantumu Mzamili Zodo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi ni kweli kwamba Serikali kwa kujali na kuthamini afya za wananchi imeendelea kujenga, kukarabati na kutanua vituo vya huduma za afya ili kusogeza huduma bora za afya kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuzingatia hilo, Serikali pia imeweka mkakati wa kuhakikisha kasi ya ujenzi wa vituo vya huduma za afya kote nchini inaendana na kasi ya ajira za watumishi ili kuviwezesha vituo hivyo kuanza kutoa huduma za afya katika vituo vyote vinavyojengwa na kukamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndio maana katika kipindi cha mwaka 2017 hadi 2020 jumla ya watumishi takribani 12,868, wastani ya watumishi 4,200 kila mwaka wameajiriwa lakini hivi sasa Serikali inaendelea na ajira za watumishi 2,726 ambazo pia zitakwenda kupunguza upungufu wa watumishi katika vituo vyetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuhakikisha kwamba tunaajiri watumishi katika vituo hivyo, ahsante sana.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza: - Sekta ya Afya nchini ina upungufu wa Watumishi wapatao 16,000:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na changamoto hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa hii nafasi. Napenda kuuliza swali langu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na upungufu huo wa watumishi wa afya kwenye hivi vituo kwa nini Serikali isitoe vibali maalum kwa hizi zahanati na vituo vya afya kuajiri watumishi wa kujitolea kwa kutumia mapato yao ya ndani, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA(MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua kwamba pamoja na jitihada za Serikali Kuu kuajiri watumishi katika Sekta ya Afya lakini mamlaka za Serikali za Mitaa zina wajibu pia wa kuajiri watumishi hawa kwa mikataba kupitia mapato ya ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hili naomba nimhakikishie kwamba Serikali ilikwishatoa kibali kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kupitia zahanati, vituo vya afya na hospitali wale ambao mapato yao yanaruhusu kuajiri watumishi kwa mikataba, waajiri na Serikali imeendelea kufanya hivyo; kuna vituo vingi ambavyo vina watumishi wa mkataba wanaolipwa na Halmashauri ili kuboresha huduma za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hivyo, naomba nimhakikishie kwamba suala hilo lipo hivyo na niwaelekeze Wakurugenzi wote wa Mamlaka za Serikali za Mitaa vile vituo ambavyo vina uwezo wa kuajiri watumishi wenye sifa kwa kufuata taratibu, waajiriwe kuhakikisha kwamba tunaboresha huduma za afya katika vituo vyetu, ahsante sana.