Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 50 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 411 2021-06-14

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza: -

Sekta ya Afya nchini ina upungufu wa Watumishi wapatao 16,000:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na changamoto hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA(MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Mzamili Zodo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa Sekta ya Afya nchini ina upungufu wa watumishi ambapo hadi mwezi Mei 2021 watumishi waliokuwepo ni asilimia 41 ya mahitaji halisi. Upungufu huo unatokana na sababu mbalimbali ikiwemo kustaafu kazi, kufariki na kuongezeka kwa idadi ya Vituo vya kutolea huduma za afya nchini kutokana na utekelezaji wa Programu ya Ujenzi na Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia mwaka 2017 hadi 2020 Serikali kwa kushirikiana na wadau imeajiri watumishi 12,868 wa Sekta ya Afya ambao wamepangwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Adha, Serikali inakamilisha taratibu za ajira 2,726 za watumishi wa kada mbalimbali za afya zilizotangazwa Mwezi Mei 2021. Watumishi hao watapangwa kwenye Vituo vya kutolea huduma za afya vyenye uhitaji mkubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ili kukabiliana na changamoto hii, mpango wa Serikali ni kuendelea kuajiri watumishi wa kada za afya kwa awamu, nashukuru.