Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha kazi ya kupeleka umeme vijiji 49 vya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ambavyo bado haijapatiwa umeme?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri tuishukuru Serikali kwa kazi ambayo imeanza kwenye vile vijiji vichache viwili ambavyo vilikuwa vimepitiwa na umeme mkubwa, lakini kwa hivi vijiji 47 kwa kuwa tunategemea Mradi wa REA, kazi hii Mheshimiwa Naibu Waziri imekuwa na changamoto kidogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kupata majibu ya Serikali sasa ni lini kazi za kupelekea umeme kwenye vijiji hivi vyote vilivyobaki itaanza na kukamilika kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa Jimbo la Korogwe?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili kwenye Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko ule wa Kwanza tulipeleka umeme kwenye vijiji, lakini maeneo mengi ya vijiji bado hajafikiwa na kwenye mzunguko huo wa pili tunafikiria kupeleka kwenye kilometa moja kwenye kila kijiji.

Ni upi mpango sasa wa Serikali kwa vile vijiji vya mzunguko ule wa kwanza na ule mzunguko wa pili kukamilisha maeneo yote ya vijiji ili wananchi wa vijiji vyetu waweze kupata huduma hii ya umeme? Nashukuru sana.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika majibu ya msingi kwamba upelekaji wa umeme kwenye vijiji vyote 49 na hivyo viwili tayari kazi imeanza, itakamilika ifikapo Septemba, 2022 na niseme ni kwa Korogwe Vijijini peke yake lakini katika maeneo yote ambayo vile vijiji tulikuwa hatujavipelekea umeme tayari kazi hizi zimeanza na tutahakikisha kwamba ndani ya huo muda tuliousema ambao maximum ni Disemba, 2022 vijiji vyote kama 1,500 vilivyobakia vitakuwa vimepata umeme na tutahakikisha kwamba kila mtu anapata manufaa ya umeme huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika swali la pili ni kweli kwamba mpaka sasa hatujatosheleza kupeleka umeme katika vitongoji vyote kwenye maeneo yote, lakini maendeleo ni hatua, tulianza hatuna kabisa, sasa tumepeleka robo, baadaye nusu, sasa kwenye vijiji tunaenda kumaliza. Niwaahidi tu Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali inayo nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba katika vitongoji pia tunafikisha umeme kwa kadri inavyowezekana, na kama tulivyokuwa tunasema kwenye vitongoji tunapeleka kupitia hiyo REA, lakini huko mradi maalum wa kupeleka umeme kwenye vitongoji unaoitwa densification, lakini pia TANESCO ni jukumu lao la kila siku kuhakikisha wanapeleka umeme katika maeneo hayo, ni wahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba tutaendelea kupeleka umeme katika maeneo yote ya nchi yetu ya Tanzania.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha kazi ya kupeleka umeme vijiji 49 vya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ambavyo bado haijapatiwa umeme?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naomba kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunahitimisha mahojiano na Waziri akatuambia kwenye utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu vijiji vyote vinakwenda kupata umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, kinachoendelea kwenye vijiji vyetu na majimbo yetu ni mchakato ambao haueleweki kwa wananchi kwa sababu walimsikia Waziri akisema kila nyumba, kila kijiji na kila kitongoji kinakwenda kupata umeme. Kinachoendelea kwa wakandarasi walioki site sasa wanafanya survey wanasema kila kijiji wanapelekea nyumba 20 tu, sasa hii imeleta changamoto kwetu sisi Wabunge hasa tunaotoka vijijini.

Ni nini kauli ya Serikali wao ili wawaeleze wananchi ni nyumba zote vijiji vyote au tunakwenda awamu kwa awamu? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ashatu Mbunge wa Kondoa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba nia ya Serikali ni kuhakikisha kwamba kila Mtanzania anapata umeme nyumbani kwake, lakini haiwezi kuwezekana kufanya hivyo kwa siku moja na tunapotoa kazi kwa mkandarasi kulingana na bajeti na fedha tuliyonayo tumekuwa tukianza na wale tunaowaita wateja wa awali kwa hiyo mkandarasi tunampa kazi ya kupeleka umeme katika eneo fulani, na kwenye mkataba wake tunampa labda wananchi 100 au 500 au 700 kulingana na wigo wa lile eneo lilivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, na mkandarasi akikamilisha hao watu 500 sisi tunafunga mkataba wa mkandarasi kwamba tunamaliza.

Sasa kinachokuwa kimebakia ni kwamba wananchi wa maeneo yale sasa waendelee kufuatilia na kuomba umeme kutoka taasisi yetu ya umeme yetu ya TANESCO ili waendelee kuunganishiwa kwa sababu sio watu wote wanakuwa tayari kuunganishiwa umeme katika siku moja ambapo mkandarasi anakuwepo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa maelezo mafupi ni kwamba mkandarasi anakuwa na wateja wa awali wa kuanza nao na akikamilisha wale aliopewa wateja wengine wanaendelea kupewa umeme na TANESCO na tutahakikisha kwamba kila Mtanzania anapata umeme nyumbani kwake. (Makofi)

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha kazi ya kupeleka umeme vijiji 49 vya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ambavyo bado haijapatiwa umeme?

Supplementary Question 3

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Serikali itakamilisha kupeleka umeme katika vijiji vya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda, vijiji ambavyo viko katika Kata ya Kakese, Kijiji cha Kamakuka, lakini katika Kata ya Mwamkulu vijiji kama Saint Maria, Kawanzige, Mkwajuni na Ikokwa, lakini katika Kata ya Kakese, Kijiji cha Songebila? Ahsante. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Martha Mariki, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Katavi kwamba vile vijiji vyote alivyovitaja kikiwemo cha Saint Maria ambayo nimekisia vizuri vyote viko katika mpango wa REA III Round II na tayari mkandarasi ameshaaza kazi katika maeneo hayo tunamshukuru kwa sababu yeye na Mheshimiwa Pinda wamekuwa wakifuatilia na tunahakikisha kwamba kabla ya Disemba mwakani tayari vijiji hivyo vitakuwa vimepata umeme kwa ile programu tuliyoiweka ya mkandarasi kuhakikisha anapeleka umeme katika muda huo.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha kazi ya kupeleka umeme vijiji 49 vya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ambavyo bado haijapatiwa umeme?

Supplementary Question 4

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa licha ya Kata ya Lukulaijo kuwa jirani na Kata ya Nkwenda ambayo ni mjini bado kuna vijiji viwili ambavyo havina umeme ambayo ni Kijiji cha Mgorogoro lakini na Kijiji cha Mkombozi, nataka nijue commitment ya Serikali kwa sababu vile vijiji havipo mbali; ni lini vitapelekewa umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya katika maswali ya nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa Mheshimiwa Anatropia, vijiji vyote na mitaa yote ya mjini pamoja na maeneo ambayo ni Mgorogoro pamoja na Lukulaijo na maeneo mengine ambayo yamebaki tumesha-design mkandarasi wa peri-urban ambaye ataanza kupeleka umeme mwezi ujao, na ndani ya miezi tisa atakamilisha maeneo yote ya kwa Mheshimiwa Mbunge watakuwa wameshapekewa umeme. (Makofi)

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha kazi ya kupeleka umeme vijiji 49 vya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ambavyo bado haijapatiwa umeme?

Supplementary Question 5

MHE. KABULA E. SHITOBELO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Je, ni lini Serikali itakamilisha kazi ya kupeleka umeme katika vijiji vya Mkoa wa Mwanza kama Nyanchenche -Segerema; Nyakafungwa - Buchosa; Gulumungu - Misungwi; Kawekamo, Mwambogwa, Kwimba na Ilemela?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama ambavyo nimeeleza katika majibu ya muda uliopita na Mheshimiwa Naibu Waziri ulivyosema Mkoa wa Mwanza umebakiza vijiji 121; lakini yako maeneo ambayo ameyataja Mheshimiwa Mbunge maeneo la Ilemela, Nyamagana, Nyamadoke, Nyamongolo pamoja na maeneo yote ya Rwanima tutawapekelea umeme mwezi disemba mwaka unaokuja.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimpe tu taarifa Mheshimiwa Mbunge kwamba Mwanza tumepeleka wakandarasi wa aina mbili; wakandarasi wa peri-urbun wanaendelea na maeneo uliyotaja, lakini kuna maeneo ya vitongoji ambayo yana-cover Sengerema mpaka Buchosa ambao wakandarasi wameshafika site tayari. (Makofi)