Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 48 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 402 2021-06-09

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha kazi ya kupeleka umeme vijiji 49 vya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ambavyo bado haijapatiwa umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji 49 vilivyobaki katika Wilaya ya Korogwe ilianza mwezi Mei, 2021 na kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivi itakamilika ifikapo mwezi Septemba, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya utekelezaji wa mradi huu inahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 urefu wa kilometa 289.4, njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4 urefu kilometa 45, ufungaji wa transfoma 50 zenye uwezo wa KVA 50 pamoja na kuunganisha huduma ya umeme wateja wa awali 990. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 12.85.