Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Singida ili ndege za ATCL zianze kutua na kurahisisha usafiri?

Supplementary Question 1

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikushukuru sana na kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza pia kukuona umekaa kwenye hicho kiti kwa kweli kimeku-fit sawasawa. Kama Mbunge kijana nakupongeza sana, hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la nyongeza ni kwamba imekuwa ni habari kwa kweli ya muda mrefu sana, wananchi wa Mkoa wa Singida tumeendelea kupata ahadi, ahadi, ahadi ambazo kwa kweli kimsingi ningependa sana kaka yangu na mtani wangu ninaye muheshimu sana watupe commitment kama Serikali; uwanja huu wa ndege wa Mkoa wa Singida. ambao kimsingi tuko jirani kabisa na Makao Makuu ya nchi lini Serikali inakwenda kuanza ujenzi wa uwanja huu kwa maslahi ya wananchi wa Mkoa wa Singida? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nataka nipate commitment. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Immanuel Kingu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza katika ujenzi wa uwanja wa ndege au kama ilivyo kwenye barabara tayari uwanja huo umefanikiwa kupata hatua ya kwanza. Tumesema usanifu na upembuzi yakinifu umeshafanyika; maana yake tayari hapa tulipo tunajua angalau inahitajika gharama kiasi gani. Tunatafuta mapato ya ndani, lakini pia na washirika wetu wa maendeleo. Tukipata fedha hata kesho Mheshimiwa Kingu, uwanja huu utaanza kujengwa.

Naomba nikuhakikishie kwa niaba ya Serikali kwamba tuna nia ya dhati kwamba kila Makao Makuu ya Mkoa kuwe na uwanja wa ndege ili uweze kutoa huduma katika maeneo yale. Kila Mheshimiwa Mbunge angeweza kupenda baada ya Bunge kuahirishwa apande ndege itue nyumbani kwake kwenye mkoa wake, achangie mapato, lakini pia na wageni wengine wapate huduma kirahisi sana. Ahsante.

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Singida ili ndege za ATCL zianze kutua na kurahisisha usafiri?

Supplementary Question 2

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Kwa kuwa uhitaji wa uwanja wa ndege Mkoa wa Singida ni sawa na uhitaji wa uwanja wa ndege Mkoa wa Simiyu na tumekuwa tukipata majibu kwamba Serikali iko kwenye mchakato.

Sasa na mimi nataka tu commitment kwamba je, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege Mkoa wa Simiyu pale Igegu ili wananchi waweze nao kupanda ndege nikiwemo na mimi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye swali la Mheshimiwa King una kwa kuwa mkoa huu ni mkoa mpya, Mkoa wa Simiyu na usanifu wa kina na upembuzi yakinifu umeshafanyika, gharama zimeshajulikana, Serikali inatafuta vyanzo mbalimbali, tukipata fedha Mheshimiwa Mbunge wa Busega naomba nikuhakikishie kwamba utapata uwanja katika Mkoa wa Simiyu. Kama ambavyo ameanza mapema lakini wanafanya kubwa sana. Hongereni sana kwa kazi nzuri ambayo mnafanya katika mkoa huo. Ahsante sana.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Singida ili ndege za ATCL zianze kutua na kurahisisha usafiri?

Supplementary Question 3

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona; kwa kuwa Mkoa wa Njombe nao ni mkoa mpya na kwa kuwa uwanja wa ndege upo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na kwa kuwa Njombe tumekuwa tukilima sana maparachichi.

Swali, ni lini Serikali itaanza kutekeleza kuujenga uwanja wa ndege katika Mkoa wa Njombe na kwa sababu Mbunge amekuwa akiuliza mara nyingi sana Mbunge Mwanyika juu ya uwanja wa ndege? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge mzoefu na maarufu katika Bunge hili tukufu; ni kweli kwamba Mkoa huu ni mkoa mpya na ni maarufu kwa kilimo cha maparachichi ambayo pia sasa hivi yamepata soko nje ya nchi. Wanahitaji uwanja wa ndege ili maparachichi yale yatoke moja kwa moja Njombe yaende popote ambapo yanahitajika huko duniani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema ana bahati kwamba eneo lake hili usanifu umeshafanyika, gharama zimeshajulikana na kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais Mama Samia kwamba Watanzania walipe kodi bila shuruti, pamoja na vyanzo vingine tukipata fedha za kutosha hata kesho tutajenga uwanja huu. Ahsante.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Singida ili ndege za ATCL zianze kutua na kurahisisha usafiri?

Supplementary Question 4

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwa kuwa ipo barabara ambayo ilitolewa ahadi na hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, barabara ya Kibamba – Mpiji – Mabwepande na tayari bajeti ya Wizara hii imepita.

Sasa nataka kauli ya Serikali juu ya bajeti husika juu ya barabara hii; ni nini kimefanyika juu ya utengenzaji wa barabara hii katika mwaka huu ikitegemea Hayati alisema wapelekewe kwa udharura?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba bajeti yetu imepitishwa tarehe 27 na 28 Mei, 2021 hapa Bungeni tunawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge kwa kupitisha bajeti yetu. Tunaomba tuwahakikishie kwamba ahadi zote za viongozi wakuu, Mheshimiwa Rais Hayati Magufuli, Mama Samia aliyepo madarakani sasa, Mheshimiwa Waziri Mkuu na ambazo zimetajwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi zitatekelezwa. Tupeane muda tu. Mheshimiwa Mbunge, tutapitia kwa haraka haraka tuweze kujua ni barabara gani zimetajwa, zipo nyingi nchi nzima. Siwezi kukudanganya hapa lakini tukipitia kama ipo na fedha yake imetengwa tutaisimamia na kazi itafanyika na bahati nzuri tumepanga kwamba eneo hilo tutoe malalamiko mkoa wa Dar es Salaam, tumewekeza fedha za kutosha kuboresha barabara ili uchumi wa Tanzania uendelee kuku ana fedha hizo zifanye kazi za kujenga uchumi wa Watanzania kutoa huduma za kijamii. Ahsante sana.