Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 47 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 393 2021-06-08

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Singida ili ndege za ATCL zianze kutua na kurahisisha usafiri?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Elibariki Immanuel Kingu, Mbunge wa Singida Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanja cha ndege cha Singida ni miongoni mwa viwanja 11 vilivyofanyiwa Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina kwa ufadhili wa fedha kupitia mradi wa Benki ya Dunia. Viwanja hivyo 11 ni kama ifuatavyo; Lake Manyara, Musoma, Songea, Kilwa Masoko, Tanga, Iringa, Lindi, Moshi, Singida, Njombe na Simiyu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hatua ya awali ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina kukamilika, Serikali imejipanga kuanza hatua ya ujenzi kwa viwanja vyote vya ndege kwa awamu kwa kutumia fedha za ndani kutokana na ukweli kwamba gharama za ujenzi wa viwanja hivyo ni kubwa ukilinganisha na bajeti inayotolewa kila mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia bajeti, Serikali kupitia TANROADS imejipanga kuanza na ujenzi wa viwanja vya Iringa na Songea. Ujenzi wa viwanja vilivyobaki kikiwemo cha Singida utaanza mara Serikali itakapopata fedha. Aidha, kwa sasa Serikali inaendelea kuwasiliana na washirika wa maendeleo ili kuweza kupata fedha za kujenga viwanja hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maelezo hayo hapo juu, namuomba Mheshimiwa Elibariki Immanuel Kingu na wananchi wa Singida waendelee kuvuta subira kwani Serikali ya Chama cha Mapinduzi ina nia ya dhati ya kujenga kiwanja hicho cha Singida. Ahsante.