Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Mahakama ya Mwanzo katika Tarafa ya Mambwenkoswe ili kuwapunguzia wananchi adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta haki?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri yanayotia matumaini ya Serikali, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hizi Tarafa ambazo zimetajwa zenye Mahakama kwa maana ya majengo; Mahakama kujenga ni jambo moja na kutoa huduma ni jambo la pili: Je, Serikali ipo tayari kuhakikisha kwamba Mahakimu wanakuwepo muda wote katika hizi Tarafa nne ambazo zina Mahakama tayari? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mahakama ya Wilaya ya Kalambo sasa hivi wanatumia jengo la CCM na hivyo sisi kama CCM tunaona kama wanatunyima mapato: Je, Serikali ipo tayari katika mpango wa kujenga Mahakama za Wilaya, Wilaya ya Kalambo ikapewa kipaumbele kujenga Mahakama ya kisasa yenye kulingana na hadhi ya Wilaya yetu? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, napenda kumjibu Mheshimiwa Kandege, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza linahusu masuala ya watumishi, Mahakimu. Ni mpango wa Mahakama kuendelea kuongeza idadi ya Mahakimu ili waweze kutosheleza ingawa kwa kweli bado watumishi ni tatizo kubwa katika sekta mbalimbali hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, suala la pili ni la kuhama kwenye majengo ya CCM na kurudi kwenye majengo ya Mahakama. Kama nilivyoeleza kwenye jibu langu la msingi ni kwamba tunao mkakati ambao kufikia 2025/2026 nchi nzima, Makao Makuu ya Wilaya zote yatakuwa na majengo mapya ya Mahakama zetu na Makao Makuu ya Tarafa zote nchini yatakuwa yamepata hayo majengo. Kwa hiyo, namwomba tu Mheshimiwa awe mvumilivu kidogo. Ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Mahakama ya Mwanzo katika Tarafa ya Mambwenkoswe ili kuwapunguzia wananchi adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta haki?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Najua Serikali mna mkakati wa kujenga Mahakama kila Wilaya. Wilaya ya Bunda haina jengo la Mahakama, imepanga kwenye nyumba ya Mzee Wasira muda mrefu, sasa hivi wamehamia kupanga eneo lingine. Ahadi mlitoa tangu enzi ya Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe akiwa Waziri wa Katiba na Sheria. Nataka kujua ni lini Mahakama ya Wilaya ya Bunda itajengwa ya kwao?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, napenda kumjibu Mheshimiwa Ester Bulaya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kama mnavyofahamu nchi inapitia changamoto mbalimbali. Kwa sasa kama nilivyoahidi, kufikia 2025 sehemu zote ambazo hazina Mahakama za Wilaya na Makao Makuu ya Tarafa zote katika ngazi ya Kata zitakuwa na majengo mapya. Tuvumilie, tutaendelea kuazima majengo lakini mwisho wetu tumeuweka kwenye 2025 iwe ni mwisho wa habari hii. Ahsante.