Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 46 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 383 2021-06-07

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Mahakama ya Mwanzo katika Tarafa ya Mambwenkoswe ili kuwapunguzia wananchi adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta haki?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kalambo ina Tarafa tano ambazo ni Mambwenkoswe, Matai, Mwimbi, Kasanga na Mwazye. Kati ya hizo, ni Tarafa nne ambazo zina huduma ya Mahakama ya Mwanzo isipokuwa Tarafa ya Mambwenkoswe.

Mheshimiwa Spika, Mahakama ya Tanzania inao Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Miundombinu ya Mahakama wa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) ambao unajumuisha mahitaji yote ya ujenzi na ukarabati wa Mahakama katika ngazi zote za Mikoa, Wilaya na Makao Makuu yote ya Tarafa nchini.

Mheshimiwa Spika, napenda kumwahidi Mheshimiwa Mbunge kuwa katika kipindi hicho Tarafa yake hiyo moja iliyosalia pia itazingatiwa katika mpango huo. Ahsante.