Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA K.n.y. MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kubadili Shule za Msingi za Tarafa ya Ngorongoro kuwa bweni ilikunusuru maisha ya wanafunzi ambao wamekuwa wakitembea umbali mrefu na kuhatarisha maisha yao kutokana na wanyamapori kwani eneo kubwa la Tarafa hiyo ni sehemu ya hifadhi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwanza nitangulize shukrani za pekee kwa sababu Serikali yetu imeendelea kutambua umuhimu wa kujenga shule za bweni katika wilaya za wafugaji ambapo kwa wastani mtoto hutembea hadi kilometa 13 kwa siku kufika shuleni.

swali langu la kwanza; kwa kuwa kuna shule kadhaa za bweni kongwe ikiwepo Shule ya Bweni ya Longido ambayo ilikuwepo kabla ya uhuru na ya Keitumbeine, Serikali ina mpango gani wa kuzikarabati shule hizi za msingi ambazo baadhi ya miundombinu yake ni chakavu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa idadi ya watu inaendelea kuongezeka na hizi shule za bweni tulizonazo za msingi zinazidi kuwa ndogo, Serikali ina mpango gani wa kuongeza miundombinu ya madarasa na nyumba za walimu na mabwalo ili watoto waendelee kusoma katika mazingira mazuri na rafiki? Ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika,
ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kiruswa, Mbunge wa Longido kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza la msingi amejaribu kuainisha kwamba mpango upi wa Serikali wa kuhakikisha tunakarabati shule kongwe za msingi nchini. Wakati tunapitisha bajeti yetu moja ya jambo ambalo tulizungumza hapa Bungeni ni kwamba tumeshazitambua shule 726 kongwe zilizojengwa kabla ya uhuru na zile ambazo zilijengwa mara baada ya uhuru ambazo zimechakaa.

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali sasa hivi ni kutafuta fedha kuhakikisha kabisa kwamba tunazikarabati shule zote kongwe na ahadi ya Serikali ipo palepale kwamba tutazikarabati ikiwemo Shule ya Msingi ya Longido ambayo Mheshimiwa Mbunge ameieleza.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, mpango mkakati wa Serikali ni upi kutokana na ongezeko la idadi ya watu na linapelekea wanafunzi vilevile kuongezeka hususan katika kujenga mabweni, mabwalo na madarasa ya kisasa. Kama nilivyoeleza awali kwamba na Wabunge wote ni mashahidi katika hili, kwamba sasa hivi Serikali tumekuwa tukijenga au tukikarabati mabweni, madarasa pamoja na miundombinu mingine ambayo inaboresha elimu hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kabisa kwamba bado tuna mipango mingi. Miongoni mwa mipango tuliyonayo sasa hivi, tuna mpango mpya wa shule bora, lakini vilevile tuna mpango wa BEST, SEQUIP na EQUIP. Mipango ipo mingi sana, yote lengo lake ni kuhakikisha kwamba tunaongeza miundombinu mashuleni na kuboresha miundombinu ya elimu nchini.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Wabunge wote waondoe wasiwasi, Serikali ya Awamu ya Sita tutahakikisha tunawafikia wote katika Majimbo yao. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA K.n.y. MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kubadili Shule za Msingi za Tarafa ya Ngorongoro kuwa bweni ilikunusuru maisha ya wanafunzi ambao wamekuwa wakitembea umbali mrefu na kuhatarisha maisha yao kutokana na wanyamapori kwani eneo kubwa la Tarafa hiyo ni sehemu ya hifadhi?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Ni kweli kwamba katika Wilaya ya Karatu, Tarafa ya Eyasi kuna Shule ya Msingi Endamaghan ambayo ni maalum kwa ajili ya hawa watoto wa kifugaji kwa maana ya Wahadzabe ambao wanatoka kwenye hii Tarafa ya Eyasi, lakini wapo wengine wanatoka Wilaya ya Mbulu, lakini shule hiyo ni ya muda mrefu inahitaji marekebisho kimiundombinu ili hawa wanafunzi waweze kupata hiyo huduma muhimu ya elimu. Je. Serikali sasa ipo tayari kutazama shule hiyo na kuipatia fedha kwa ajili ya maboresho hayo? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tunalichukua jambo hilo na tutafanya marekebisho na tutaboresha hiyo shule. Ahsante. (Makofi)