Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 379 2021-06-07

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA K.n.y. MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kubadili Shule za Msingi za Tarafa ya Ngorongoro kuwa bweni ilikunusuru maisha ya wanafunzi ambao wamekuwa wakitembea umbali mrefu na kuhatarisha maisha yao kutokana na wanyamapori kwani eneo kubwa la Tarafa hiyo ni sehemu ya hifadhi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Shule za Msingi za Tarafa ya Ngorongoro kuwa za bweni. Serikali kwa kushirikiana na wananchi na wadau mbalimbali wa elimu imeanzisha shule tatu za bweni ambazo ni Nainokanoka, Enduleni na Olbalbal zenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 1,014 wakiwemo wavulana 590 na wasichana 424. Shule hizo zinachukua wanafunzi wanaotoka maeneo ambayo yana wanyama wakali na yaliyo mbali na maeneo ya shule na hivyo kuwawezesha wanafunzi kuhudhuria masomo bila vikwazo vyovyote.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuongeza mabweni katika shule hizo ili kuziwezesha kuchukua wanafunzi wengi zaidi.