Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Majengo ya Mahakama za Mwanzo katika Kata za Nkoanrua na Nkoaranga ambazo majengo yake yamebomoka?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nitaomba kuuliza swali moja la nyongeza, ila naomba pia kwamba Serikali isiwe inatoa majibu tu kwa ajili ya kutuliza Wabunge, lakini kwa kweli ije na kutekeleza yale ambayo wanayasema kwenye majibu yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu; jiografia ya Jimbo langu la Arumeru Mashariki ni ngumu, kwa maana ya kwamba Mlima Meru ambao ni mlima mrefu wa pili hapa nchini uko katikati ya jimbo na kuwafanya wananchi walioko Mashariki na Kaskazini mwa mlima huo, kupata shida kufuata huduma ambazo zinapatikana Kusini mwa mlima pamoja na kufika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Je, sasa hivi Serikali haioni kwamba ni muhimu sasa kujenga Mahakama ya Mwanzo Kata ya Ngarananyuki ili wananchi walioko Kaskazini mwa mlima huo waweze kupata huduma za Mahakama? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, tuko kwenye mkakati maalum wa kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 2025/2026 nchi nzima itakuwa imefikiwa na Mahakama za Mwanzo kwenye ngazi za Makao Makuu ya Tarafa zote.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la Ngarananyuki kupata Mahakama, tunalichukua ingawa katika kipindi hiki cha fedha ambacho tunakijadili sasa kilishapita, tutalipa umuhimu kwenye kipindi kijacho cha fedha. Ahsante sana.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Majengo ya Mahakama za Mwanzo katika Kata za Nkoanrua na Nkoaranga ambazo majengo yake yamebomoka?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. naomba kuuliza swali dogo la nyongeza kwa niaba ya wananchi wa Makete.

Mheshimiwa Naibu Waziri Tarafa ya Ikuo haina huduma kabisa ya Mahakama; na ni umbali wa kilometa karibu 170 kwenda kufuata huduma ya Mahakama kwenye Tarafa ya Matamba:-

Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama kwenye Tarafa ya Ikuo kwa sababu kwa muda mrefu tumekuwa tukiomba huduma hiyo na hatujapewa? Ahsante.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi na jibu la nyongeza la Mheshimiwa, tutakuweka kwenye kipaumbele kwenye bajeti baada ya hii tunayoijadili leo. Ahsante. (Makofi)

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Majengo ya Mahakama za Mwanzo katika Kata za Nkoanrua na Nkoaranga ambazo majengo yake yamebomoka?

Supplementary Question 3

MHE. PHILIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali moja la nyongeza. Wilaya ya Songwe ni Wilaya mpya toka mwaka 2016 na nimekuwa nikiahidiwa hapa kila mwaka kwamba tutajenga Mahakama ya Wilaya, lakini mpaka sasa Serikali haina mpango wowote. Viwanja vipo, hati ipo, lakini mpaka leo hakuna jengo la Mahakama. Nirudie tena kwa mara ya tano:-

Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama katika Wilaya ya Songwe?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mulugo naomba tu asiwe na wasiwasi. Katika kipindi kijacho hiki cha fedha ambacho mmetupitishia bajeti yetu Songwe imo kwenye huu mpango. Kwa hiyo, muda mfupi ujao tutaanzisha hii miradi ya ujenzi katika eneo lake kwa kupitia fedha ambazo mmeziidhinisha wenyewe hapa.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Majengo ya Mahakama za Mwanzo katika Kata za Nkoanrua na Nkoaranga ambazo majengo yake yamebomoka?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mahakama ya Mwanzo ya Liuli ilijengwa toka kipindi cha mkoloni na ikawa imeharibika sana na kilichotokea ni Mahakama kuhama kabisa eneo hilo na kwamba shughuli za Mahakama haziendelei:-

Je, ni lini Mahakama hiyo itarejeshwa katika nafasi yake kama ilivyokuwa mwanzo hapo Liuli?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunakiri kwamba Mahakama nyingi zimechakaa. Kama nilivyoeleza katika maelezo yangu ni kwamba, mkakati wa kukarabati na kujenga majengo mapya kwenye maeneo ambayo hayana Mahakama, ukomo wake ni 2025 ambapo namwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo la Liuli tunalichukua na katika kipindi kijacho cha fedha tutahakikisha tunawasogezea hii huduma ya ukarabati wa Mahakama yao. Ahsante.

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Majengo ya Mahakama za Mwanzo katika Kata za Nkoanrua na Nkoaranga ambazo majengo yake yamebomoka?

Supplementary Question 5

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Hitaji la Nkoaranga ni sawa sawa na hitaji la Wilaya ya Buhigwe. Wananchi wa Buhigwe wanapata huduma za Mahakama ya Wilaya kwenye Wilaya nyingine ya Kasulu:-

Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kavejuru Felix, Mbunge wa Buhigwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mpango wa mwaka 2021/2022 ambao tayari bajeti yake imeshapitishwa Buhigwe ipo katika mpango wa kujengewa Mahakama ya Wilaya. Kwa hiyo, asubiri tu mageuzi kwenye eneo lake. Ahsante.