Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 44 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 376 2021-06-04

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Majengo ya Mahakama za Mwanzo katika Kata za Nkoanrua na Nkoaranga ambazo majengo yake yamebomoka?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Jengo la Mahakama ya Mwanzo Nkoanrua lilichomwa moto na wananchi na hivyo kushindwa kuendelea kutoa huduma katika eneo hilo. Aidha, jengo la Mahakama ya Mwanzo Nkoaranga katika Tarafa ya King’ori ni chakavu na hivyo kuhitaji kujengwa upya.

Mheshimiwa Naibu Spika, maandalizi ya Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Miundombinu ya Mahakama wa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) yanaendelea ambapo utajumuisha mahitaji yote ya ujenzi na ukarabati wa Mahakama katika ngazi zote. Mpango huu utaweka kipaumbele zaidi kwenye ujenzi na ukarabati wa Mahakama za Mwanzo nchini. Lengo la Mahakama ya Tanzania ni kuhakikisha kuwa Tarafa zote 570 zilizopo nchini zinakuwa na Mahakama ya Mwanzo ifikapo mwaka 2025.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa Mahakama za Mwanzo za Nkoanrua na Nkoaranga zitapewa kipaumbele katika ujenzi na ukarabati kwenye mpango huo.

Napenda kutoa wito kwa Waheshimiwa Wabunge kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa Mahakama katika maeneo yetu, kwani kitendo cha kuchoma moto majengo ya Serikali hasa Mahakama, ni kitendo cha kulaaniwa na hakipaswi kurudiwa tena. Ahsante.