Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamaliza changamoto ya Maji katika Kituo cha Utafiti na Chuo cha Kilimo Ukirigulu?

Supplementary Question 1

MHE. ALEXANDER P. MNYETI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Nasikitika sana kwamba majibu haya, ndiyo haya haya ambayo huwa yanatolewa kila mwaka. Unajua kinachouma ni kwamba, vyanzo vya maji vyote vikubwa unavyovijua vinavyopeleka maji Tabora, Nzega, Igunga, Kahama na Shinyanga vinatoka Misungwi, lakini wana-Misungwi hawapati fursa ya kupata miundombinu ya maji. Naomba nimwulize Mheshimiwa Waziri: Ni lini Chuo cha Ukiriguru na Kituo cha Utafiti kitapata maji? Kwa sababu, majibu haya, ni haya haya ya miaka yote.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kufahamu hilo.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Alexander Pastory Mnyeti, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye jibu langu la msingi, hiki nilichokijibu ndiyo mpango mkakati wa Wizara. Kama mnavyofahamu Wizara ya Maji tuko kwenye mpango mkubwa sana wa mageuzi. Hivyo, tuache kuangalia mambo yaliyopita, tuangalie ya sasa hivi na utekelezaji wetu sisi ambao tuko, nafikiri mnauona. Kwa hiyo, napenda tu kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, suala hili la maji katika hiki chuo mwaka ujao wa fedha kazi zinakuja kutekelezwa kadiri ya mipango ilivyo ndani ya Wizara.