Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 44 Water and Irrigation Wizara ya Maji 375 2021-06-04

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itamaliza changamoto ya Maji katika Kituo cha Utafiti na Chuo cha Kilimo Ukirigulu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alexander Pastory Mnyeti, Mbunge wa Misungwi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Utafiti na Chuo cha Kilimo Ukirigulu kilikuwa na Skimu ya Maji iliyojengwa mwaka 1965. Chanzo cha maji cha skimu hiyo ni Ziwa Victoria na ina matenki mawili ya maji. Moja lipo Kijiji cha Mwalogwabagole na lingine liko eneo la chuo hicho. Skimu hiyo ina vituo vya kuchotea maji 15.

Mheshimiwa Naibu Spika, usanifu wa mradi kwa ajili ya ukarabati wa skimu hiyo umekamilika na katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetenga shilingi 630,733,364 ili kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji na kutahusisha ulazaji wa mabomba mapya kilometa 40.4 na ukarabati wa matenki mawili katika Kituo cha Ukirigulu na Kijiji cha Mwalogwabagole yenye lita za ujazo 225,000. Chuo cha Ukirigulu pamoja na Vijiji vya Mwalogwabagole, Buganda, Nyagholongo, Ngudama, Nyamule, Mwagala, Nyamikoma vitanufaika baada ya kukamilika kwa mradi na ukarabati wa skimu hiyo na jumla ya wananchi 19,658 watanufaika.